ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 19, 2018

KIAPO CHA MAHARUSI | ROYAL WEDDING: HARRY AND MEGHAN EXCHANGE VOWS

   GSENGOtv  
Imekusongezea matukio yaliyojiri sanjari na yale yaliyojiri hii leo kwenye harusi ya mjukuu wa himaya ya Malkia Elizabeth. 

Katika harusi hiyo maandalizi muhimu yote yalifanywa na kukamilika mapemaa, ulinzi ukizingatiwa kila sekunde kwaajili ya kuhudumia wageni takribani 2500 waliodhuru jijini London kushiriki shughuli hiyo wakiwemo marafiki wa karibu wa Meghan kutoka nchini Marekani na Canada, pamoja na askari na marafiki wa karibu wa Harry .

Bi Meghan Markle na Mwanamfalme Harry wamevishana pete na kutangazwa kuwa mume na mke Windsor Castle katika sherehe inayofuatiliwa na mamilioni ya watu kupitia runinga, mtandao na redio.

Wawili hao walifunganishwa katika ndoa mbele ya Malkia na wageni 600 waliokuwemo ndani ya kanisa la St George, katika Windsor Castle.

Bi Markle alikuwa amevalia vazi la harusi lililoshonwa na fundi mbunifu wa mitindo Mwingereza Clare Waight Keller.

Bi Meghan alitumia gari aina ya Rolls Royce Phantom kufika kanisani ambapo alipokelewa kwa shangwe na nderemo aliposhuka kutoka kwenye gari hilo na kuingia kanisa la St George.

Miongoni mwa wageni waliofika ni nyota wa televisheni Marekani Oprah Winfrey na mwigizaji Idris Elba.
George na Amal Clooney, David na Victoria Beckham pamoja na Elton John pia wamewasili.

Mwanamfalme Harry na Meghan Markle baadaye walipitia kwenye mji wa Windsor kwa msafara kwa kutumia kigari maalum cha kuvutwa na farasi.

Harry, ndiye aliyeyemsindikiza Bi Markel kwenda kwenye madhabahu baada ya babake Thomas kushindwa kuhudhuria harusi hiyo kutokana na sababu za kiafya.

Mkesha wa harusi, Mwanamfalme Harry, 33, aliambia umati wa watu Windsor kwamba anajihisi "mtulivu" na kwamba Bi Markle, 36, anajihisi "vyema sana".

Katika kiapo chake cha ndoa, Bi Markle hakuahidi "kumtii" mume wake. Mwanamfalme Harry ameamua kuwa na pete ya ndoa.

Wageni 600 walifuatilia harusi hiyo, ambayo iliongozwa na Askofu Mkuu wa Canterbury, Justin Welby, katika kanisa la St George.

Umati wa watu wakiungana na waandishi wa habari kutoka maeneo mengi duniani wamlikusanyika Windsor kwa sherehe hii kubwa.

Inakadiriwa kwamba watu hadi 100,000 walikuwa kwenye barabara za mji huo.
Watu wa kawaida 1,200, wengi ambao wametambuliwa kwa juhudi zao za hisani katika jamii, walialikwa kuhudhuria harusi hiyo Windsor Castle.

Bi Markle alikuwa na mabinti 10 wapamba harusi na wavulana, wote wa chini ya miaka minane, wakiwemo Mwanamfalme George na Bintimfalme Charlotte.

Bi harusi alilakiwa na Mwanamfalme Charles, ambaye alimtembeza hadi kwenye madhabahu.

Wakati wa ibada, wawili hao walikula kiapo kila mmoja akijitoa kwa mwenzake na kusema: "kwa mema, kwa mabaya, kwa ujatajiri, kwa umaskini, kwa ugonjwa na kwa afya, kukupenda na kukuenzi, tangu kifo kitutenganishe."

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.