ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 17, 2018

MWANAMUZIKI WA SUPER KAMANYOLA ALIYETOKA KWA MUUMINI MWINJUMA AFUNGA NDOA

GSENGOtV
Saa kadhaa jumatano ya tarehe 16 May 2018 kabla ya kuingia mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani mwanamuziki Aboubakari Mangegeka wa bendi ya Super Kamanyola yenye maskani yake Villa Park Resort jijini Mwanza amefunga ndoa na Bi. Swaumu.

Ndoa ya Kiislamu imefungwa Mji Mwema jijini hapa nao marafiki wengi wakihudhuria shughuli hiyo licha ya wengi kupewa taarifa za kama vile surprise.

Mangegeka aliye na ulemavu wa kuona na mwenye kipaji cha uimbaji ambaye awali kabla ya kujiunga na bendi hiyo alikuwa akifanya kazi na bendi ya Muunini Mwinjuma Double M Sound, anadai moja kati ya vitu vilivyomvutia kwa Bi. Swaumu na hata kuamua kumuoa ni sauti ya mvuto aliyonayo binti huyo, vingine siri yake mazee.











  




Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.