ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 7, 2018

JEMBE FM, METDO NA WADAU WAKE WAMUENZI KARUME KWA KUTEMBELEA NA KUTOA CHAKULA KWA KITUO CHA KULEA WAZEE BUKUMBI.

Leo ni Tarehe 7 April 2018, tunaadhimisha Kumbukumbu ya Kifo Cha Rais wa Kwanza wa Zanzibar Abeid Aman Karume @Jembefm 93.7 kupitia kipindi chake cha muziki wa Injili yaani #JembeGospel kwa Kushirikiana na wanamuziki wa muziki huo, Wachungaji wa makanisa kadhaa ya Kipentekoste pamoja na METDO, wameitumia siku hii muhimu ya #KarumeDay kwa kuwatembelea ndugu zetu wa kituo cha Wazee wasiojiweza kilichopo Bukumbi wilayani Misungwi mkoani Mwanza na kutoa mahitaji mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 'First Lady' Mama Janeth Magufuli.

Vilevile kuipa thamani Kazi ya utumishi uliotukuka na Kuuenzi Upendo na Msisitizo wa Mshikamano aliokuwa nao Hayati Mzee Karume.

Mshikamano ulipo baina ya Tanzania na Zanzibar umeendelea kudumu sasa yapata miaka 46. 

Ni takribani miaka miwili sasa imepita tangu Mama Janeth Magufuli alipodhuru kwenye kituo hicho (mwezi March 7 mwaka 2016) ambapo aliteuliwa rasmi kuwa Mama Mlezi Mkuu wa Kituo hicho  baada ya kuhamasisha mashirika mbalimbali, watu binafsi na taasisi za kifedha kutoa michango ya vitu mbalimbali vilivyofikia thamani ya shilingi milioni 54 na kukiwezesha kituo hicho kwa chakula, malazi na mavazi.

Hivyo mpango huu umekuja kama sehemu ya kuitikia wito wa Fist lady. 

CC:- #JembeGospel @nzwallajr @gsengo @jembenijembe







PICHA ZAIDI ZAJA.................

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.