ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 2, 2018

JINSI ARSENAL WALIVYOKUTANA NA KIPIGO CHA MBWA MWIZI TOKA KWA CITY.



Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesema klabu hiyo ilishindwa na klabu iliyo bora zaidi kwa sasa Uingereza baada yao kulazwa 3-0 kwa mara ya pili katika kipindi cha wiki moja na Manchester City Alhamisi.
Gunners walikuwa wamelazwa 3-0 na City katika fainali ya Kombe la Carabao Jumapili.
Mechi ya Ligi ya Premia kati ya timu hizo mbili iliyochezwa Alhamisi iliamuliwa katika dakika 33 za kwanza kutokana na mabao ya Bernardo Silva, David Silva na Leroy Sane.
Gunners walipoteza nafasi ya kukomboa bao moja kipindi cha pili pale mchezaji waliyemnunua £56m, Pierre-Emerick Aubameyang, aliposhindwa kufunga mkwaju wa penalti kipindi cha pili.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.