ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, December 21, 2017

ANTU MANDOZA KUTIMIZA NDOTO YAKE YA KUIGIZA NA RAMSEY NOAH KUTOKA NCHINI NIGERIA

 
 Antu Mandoza akiwa katika picha ya pamoja na Muigizaji nyota wa Filamu kutoka nchini Nigeria Ramsey Noah wakiwa katika picha ya pamoja.
Mwigizaji nyota wa filamu na Mkongwe wa tasnia hiyo kutoka nchini Nigeria ,Ramsey Noah ametamani kufanya kazi na nyota mwingine wa movie anaechipukia kwa kasi katika tasnia hiyo hapa nchini,ambae ameng'ara vilivyo katika filamu ya 'KIUMENI' , Antu Mandoza wa Tanzania . 
"Anaonekana ni binti mweye kipaji,anaejiamini,kwa hakika natamani nipate muda wa kubaini kipaji chake zaidi kwa kufanya nae angalau hata filamu moja,itaweza kumsaidia zaidi kujitanua na kutambulika Kimataifa",alisema Ramsey huku akimtazama Antu kwa tabasamu laini la ucheshi.

Antu Mandoza ni Binti wa makamo hivi,lakini amejaaliwa kuwa na kipaji cha uigiza wa filamu na mwenye uthubutu wa kufanya jambo.Antu Mandoza na Ramsey Noah walikutana katika Warsha fupi iliyoandaliwa na Sahara Group iliyofanyika hotel ya Hyatt Dar Es Salaam mnamo Desemba 16 2016,ambayo pia iliwahusisha wasanii mbali mbali wa bongo movie .

 Ikiwa ni movie yake ya kwanza 'KIUMENI', Antu Mandoza amefunguka na kusema kuwa mwaka ujao utakua ni mwaka wa kazi tu, kama ilivyo Slogan ya Raisi Dkt John Pombe Magufuli,na anategemea kufanya kazi na Ramsey Noah na wasanii wengine wengi wa Ndani na Nje ya Tanzania. 

Antu alijipatia Umaarufu katika filamu ya Kiumeni aliyocheza na Ernest Napoleon,ambayo lishinda tuzo 2 ZIFF mwaka 2017.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.