ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, November 27, 2017

FUNGUKA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO HAUMUACHI MTU SALAMA CHUKUA HATUA.


Mapungufu yaliyoko katika sheria ya elimu ya mwaka 1978 yanadaiwa kuchangia kumkosesha haki mtoto wa kike pale anapoolewa kutokana na sheria hiyo kumtambua mtoto kuwa ni yule aliye katika shule ya msingi pekee.

Akizindua maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia katika mikoa ya kanda ya ziwa jijini Mwanza Mrakibu Mwandamizi wa Polisi mkoani Mwamwa ALLY MKALIPA amesema ni vigumu kuchukua hatua pale mwanafunzi wa sekondari anapopata ujauzito au kuolewa hivyo ameshauri kubadilishwa kwa sheria hiyo.

Mimba za utotoni zimeendelea kuwa kikwazo kikubwa kwa mtoto wa kike katika kutimiza ndoto ya kupata elimu.

Mkoa wa mwanza ni miongoni mwa mikoa nchini inayokabiliwa na ongezeko la mimba za utotoni.
Katika uzinduzi wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia katika mikoa ya kanda ya ziwa,baadhi ya  changamoto zinazochangia ongezeko la mimba miongoni mwa wanafunzi zikabainishwa.

Baadhi ya watendaji wa kata wakaelezea matatizo yanayochangia ongezeko la mimba za utotoni kwenye maeneo yao.

Akizindua maadhimisho hayo jijini mwanza,mrakibu mwandamizi wa polisi mkoani mwanza ALLY MKALIPA akashauri kubadilishwa kwa sheria ya elimu.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia mwaka huu ni funguka pinga ukatili wa kijinsia elimu salama kwa wote.















Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.