ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, October 12, 2017

NAIBU WAZIRI MMPYA WA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI ABDALLAH ULEGA AMEAHIDI KULIVALIA NJUGA SUALA LA WATENDAJI WAZEMBE WENYE KUKAA OFISINI

Naibu waziri mpya wa  Wizara ya mifugo na uvuvi Abdallah Ulega ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Mkuranga akifafanua jambo kwa waandishi wa habari hawapo pichani mara baada ya kumaliza kikao cha kuzungumza na watendaji wa Wilaya ya Mkuranga alipofanya ziara yake ya siku moja(PICHA NA VICTOR MASANGU,)
 Mkurugenzi mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Mkuranga  Mshamu Munde akizungumza ofisni  kwake kuhusina na migogoro ya ardhi iliyopo katika Wilaya hiyo,

Diwani wa kata ya Makamba Hassan Dunda akifafanua jambo kuhusina na migogoro ya mshamba iliyopo katika halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
 (PICHA ZOE NA VICTOR MASANGU)

NA VICTCOR MASANGU, MKURANGA

NAIBU Waziri mpya  wa wizara ya  Mifugo na Uvuvi Abdalah  Ulega amesema hawezi kulifumbia macho hata kidogo suala la baadhi ya viongozi na watendaji ambao wamekuwa na tabia ya kufanya kazi kwa mazoea kwa kukaa tu ofisini bila ya kutimiza majukumu yao   ipasavyo na kuwaagiza kuchapa kazi kwa bidii bila ya kutegeana kwa kuvitembelea vikundi  vyote vya  uvuvi na ufuga ili kuweza kusikiliza kero na kubaini  changamoto  zinazowakabili katika kutekeleza majukumu yao.

Ulega alitoa  kauli hiyo wakati alipofanya ziara yake ya kikazi ya siku moja kwa viongozi  mbali mbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, ambapo  amesema kuna baadhi ya watumishi wengine  wamekuwa ni wazembe na kusababisha kukwamisha juhudi za serikali katika kuleta  chachu ya maendeleo  hivyo ameahidi kulivalia njuga suala hilo kwa lengo la kuweza kuboresha sekta ya uvuvi na ufugaji.

Aidha Naibu Waziri huyo aliwataka maafisa uvuvi na mifugo  kuwa wazalendo na nchi yao na kuhakikisha wanazilinda  na kuzitunza rasilimali zilizopo  pamoja na   kuweka mipango  endelevu ya kutenga maeneo  maalumu kwa ajili  ya kufanyia kazi zao sambamba na kuviwezesha vikundi hivyo  katika mambo mbali mbali ikiwemo kujenga,malambo, majosho pamoja  na kuwapatia vitendea kazi.

Pia Ulega alisema kwamba  kwa sasa kipaumbele chake kikubwa ni kuhakikisha kwamba anavisaidia kwa hali na mali  kwa kuviwezesha vikundi mbali mbali  vya wafugaji na uvuvi  pamoja na kuweka mipango madhubuti ambayo itaweza kusaidia kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo katika sekta hiyo aliyopewa dhamana na Rais Dk. John Pombe Magufuli.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filbeto Sanga akizungumzia kuhusiana na suala la ardhi alisema kuwa kumeibuka kikundi cha baadhi ya  madalali ambao ni matapeli wanachukua hela za watu na kuamua kuuza  maeneo ya mashamba  ambayo tayari yana hati miliki  bila ya kufuata taratibu zozote na  kupelekea  wananchi  wenyewe  kujikuta wanakosa maeneo  kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao za kimaendeleo.

Katika hatua nyingine Mkugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Mkurunga Mshamu Munde akizungumza katika kikao cha dharura na waandishi wa habari ofisini kwake amekanusha uvumi wa taarifa zinazotolewa na  wananchi kuhusiana na shamba  linalomilikiwa na  mwekezaji wa kampuni ya Soap Allied Industry .

Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa  eneo hilo  ambalo linalalamikiwa na wananchi hao lina ukumbwa wa hekari 1750 na kuongeza kuwa kwa sasa linamilikiwa kihalali na mwekezaji huo  tangu mwaka 1988, na kupiga marufuku  wananchi wanaovamia maeneo  ya watu kiholela bila ya kuzingatia taratibu.

“Mimi kwa kweli nina shangaa sana  huu uvumi unaotokwa kwa baadhi ya wananchi kuhusiana na eneo hili, ndugu zangu waandishi eneo hili linamilikiwa kihalali, hivyo mimi ninachowaomba watu wanaolalamika kufika ofisi za mkurugenzi ili niwape ufafanuzi zaidi na sio kuanza kusababisha migogoro ambayo haina faida  hata kidogo katika Wilaya yetu ya Mkuranga nah ii tabia kwa kweli mimi siwezi kuivumilia hata kigogo nitahakikisha kwamba maeneo yote yanatolewa kwa utaratibu unaotakiwa,”alisema Mkurugenzi huyo.

Pia Mkurugenzi huyo alisema  katikia kumuunga juhudi mkono Rais wa awamu ya tano Dk. John Pombe Magufuli katika kuwa na Tanzania yenye uchumi wa viwanda wameshatenga maeneo mbali mbali kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda ambavyo vitaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa katika kukuza sekta ya viwanda na kuleta maendeleo kwa wananchi pamoja na upatikanaji wa fursa za ajira kwa vijana.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri hiyo ya Mkuranga Juma Abed na Diwani wa kata ya Makamba  Hssan Dunda hapa wanazungumzia kuhusiana na sakata hilo la mgogoro wa shamba la mwekezaji huo na  malalamiko yanayotolewa na wananchi.

Walisema kuwa kwa sasa shamba hilo linamilikiwa kihalali na mwekezaji huyo kwani alishakabidhiwa na halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga baada ya kufuata taratibu zote zinazostahili hivyo wananchi wanatakiwa kuachana na tabia ya kuvamia maeneo mengine ambayo sio yao.

VITENDO vya uvamizi wa maeneo ya mashamba pamoja na viwanja  vinavyofanywa na baadhi ya viongozi wa  na wenyeviti wa vijiji kwa kushirikiana na madalali ambao ni matapeli kwa kuvamia maeneo ambayo sio yao na kuamua kuuza  kinyemela kinyume na taratibu katika Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani vinachangia kwa kiasi kikubwa kutokea kwa migogoro kila kukicha.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.