ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, February 23, 2015

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI ATAKA WACHIMBAJI KUJIUNGA VIKUNDI ILI KUWAWEZESHA KUPATA LESENI NA MIKOPO YA FEDHA NA VIFAA


NA, PETER FABIAN, MISUNGWI. 
NAIBU Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Charles Kitwanga, amewataka wachimbaji wadogo wa Madini kujiunga katika vikundi ili kupatiwa Leseni za uchimbaji na mkopo wa fedha za ruzuku ya Sh bilioni 9 iliyotengwa na Serikali kwa wachimbaji wadogo ili kuwawezesha pia kupata vifaa vya uchimbaji

Kitwanga ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Misungwi mkoani Mwanza alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na wananchi wa vijiji vya Mwagimagi na Mwamala akiwa katika ziara ya jimboni humo na kushiriki uzinduzi wa nyumba mbili zilizojengwa na Mzawa mwekezaji wa Kampuni ya Mwamala Gold Mine na kuzikabidhi kwa mzee Jadima Nkwabi katika kijiji cha Mwamala. 

Naibu Waziri, Kitwanga alisema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imetenga Shilingi bilioni 9 ili kutoa ruzuku ya mkopo kwa wachimbaji wadogo wa madini katika maeneo mbalimbali hapa nchini kuliko na shughuli za wachimbaji ikiwa ni lengo la kuwasaidia mitaji ikiwa ni kusaidia kukuza sekta hiyo ya Madini nchini.

 “Tumelenga kuwasaidia wachimbasji wadogo hivyo ni vyema mkajiunga katika vikundi na kuomba Leseni za uchimbaji itakayowasaidia pia kupata mikopo ya fedha za ruzuku zilizotengwa na Wizara kwa wachimbaji wadogo badala ya kung’ania kuchimba kila mtu,”alisema.

 Kitwanga alisema wachimbaji mkiungana katika vikundi na kupewa Leseni, Wizara itawapatia wataalamu wa kuwasaidia kuwaonyesha sehemu zenye Madini kwenye maeneo yenu ambapo inaonyesha madini kutokuwa mbali sana ili kuwawezesha pia kupata vifaa vya uchimbaji kwa mkopo mkiwa katika vikundi vyenu ili kuwalahisishia kufanya shughuli zenu.

 “Wizara tayari imeisha toa Leseni 27 kwa wachimbaji wadogo katika maeneo ya vijiji vya Mwamazengo (7), Ishokela (7), Mwagimagi (2) na Nyang’omango (11) Wilayani hapa katika maeneo yalipatikana Madini ambapo wachimbaji wanatakiwa kuchimba kwa kufuata sheria ya Madini ya mwaka 2010,”alisisitiza.

 Awali Mwekeaji wa eneo la kijiji cha Mwamala, Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwamala Gold Mine, Sultan Mohamed, anayetaraji kuanza uchimbaji kijijini hapo alimwelea Naibu Waziri Kitwanga, akiwa mzawa na kuomba na kupokelewa kuwa mwanakijiji kwa kununua shamba ambapo sasa ameamua kujikita kuwa mchimbaji wa eneo hilo amechangia maendeleo katika kijiji hicho.

 “Kabla sijachimba nimejenga nyumba mbili za thamani ya Sh 15 na kumkabidhi mzee Nkwabi ambaye aliniuzia shamba lake ikiwa ni kumuwezesha pia kuishi katika makazi bora pia nimetoa vifaa vya ofisi ya kijiji cha Mwamala amapo nimetoa Komputa (1) na Printe yake, Kabati la kuhidhadhi mafaili (1), Mihuri ya kisasa ya Ofisi (2), Saa ya Ukutani (1), Viti 30 vya Plastiki na kutoa Mkufunzi mmoja wa Komputa,”alisema. 

Mohamed alisema kwamba kutokana na kubaliwa kuwa mwekezaji na wanakijiji hicho atafuata taratibu zote za ushirikishwaji wa jamii na kuhifadhi mazingira atakapoanza ualishaji kutoa kipaumbele cha ajira kwa vijana wa kijiji hicho kwa kufuata Sera, taratibu na sheria za Kampuni wa uchimbaji endelevu wa kisasa wa kutumia Teknolojia na kuachana na uchimbaji duni.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.