ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, August 12, 2014

MWANZA KUWA CARLIFORNIA YA TANZANIA NA SENTA YA MIKUTANO NA BIASHARA KWA NCHI ZA MAZIWA MAKUU NA KIMATAIFA

Afisa Uhusiano wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza Joseph Mlinzi akitambulisha viongozi na wageni kwenye kikao cha Katibu mkuu kiongozi balozi Ombeni Sefue jijini hapa.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza (RAS) Ndalo Kurwijila, akitoa taarifa ya mkoa kwa mgeni rasmi balozi Sefue.
Katibu Mkuu kiongozi balozi Ombeni Sefue (aliyesimama) akizungumza na watumishi wa Umma pindi alipokutana nao katika ukumbi wa Jiji mkoa wa Mwanza, wengine katika meza kuu ni Kaimu RAS Ndalo Kurwijila (katikati) na Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza Halifa Hassan Hida.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Jumanne Sagini akijibu hoja zilizo wasilishwa na watumishi katika kikao hicho. 
Watumishi kikaoni.
Wakisikiliza kwa umakini.
Wataalamu nao walihudhulia kikao hicho.
Wajumbe wa sekretarieti ya mkoa wa Mwanza.
Uwasilishaji hoja kikaoni.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya mkoa ya Sekou Toure akiwasilisha hoja za Idara ya Afya.
Wadau wa kikao kwa umakiiiini.
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Halifa Hassan Hida akitoa neno la shukurani wakati wa kufunga kikao hicho.
Picha ya pamoja.
NA PETER FABIAN, MWANZA.
SERIKALI imewaagiza viongozi wa Mkoa na Jiji la Mwanza kushirikiana na kuweka mipango na mikakati maalumu ya kuriboresha zaidii Jiji hilo, ili kuwa Habu ya Ukanda wa nchi za Maziwa Makuu na Kituo cha kimataifa cha Mikutano na Kibiashara nchini.

Kauli hiyo ilitolewa juzi na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Omben Sefue wakati walipokutana na viongozi wa Mkoa wa Mwanza wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo baada ya kupokea taarifa fupi ya Mkoa huo kabla ya kuanza ziara ya kikazi ya siku moja mkoani humo.

Akizungumza katika Ofisi wa Mkuu wa Mkoa, Balozi Sefue alisema kwamba uongozi huo kwa kushirikiana na ule wa Jiji la Mwanza unatakiwa kuanza kuandaa mipango na mikakati ya kuriboresha na kulitanua zaidi kuwa la kisasa nalenye sifa za kimataifa ili kuwa kivutio, kituo cha mikutano kwa Ukanda wa Nchi za Maziwa Makuu barani Afrika na Senta ya biashara za kimataifa.

“Ebua viongozi wa ngazi ya Mkoa kwa kushjirikiana na wenzenu wa Jiji hili muanze kuweka mipango na mikakati na muanze kuitekeleza kwa awamu, Jiji hili linakuwa kwa kasi kama mnavyoliona sasa na muanze kulifikiria litakavyokuwa kwa miaka kumi hadi ishirini ijayo kwa  kuriboresha na kulitanua zaidi, muweke mazingira mazuri yatakayowavutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi,”alisema.
 
Balozi Sefue alisema kwamba viongozi wa Mkoa na Jiji wawe na ubunifu wa mikakati itakayotekelezeka kirahisi ikiwa ni pamoja na kuendelea kuboresha Miundombinu ya barabara zake, upatikanaji wa maji safi, umeme, huduma za Afya kwa kuwa na Hospitali, Vituo vya afya,  Vyuo, Shule na huduma Mawasiliano ya uhakika na Uwanja wa Ndege wa kisasa, Usafirishaji wa majini na nchi kavu.

“Na uhakika hatutakuwa tunajadili tena habari ya Jiji la Dar es salaam hata Nairobi kama ilivyo sasa na badala yake itakuwa Mwanza, kama mtaweka vyema mipango na mikakati yenu na mkaitekeleza kwa awamu kwa usitadi wa taratibu, kanuni na sheria za Mipago Miji basi Mwanza itakuwa Habu na Senta ya Kimataifa kwa Mikutano na Biashara,” alisema.

Awali Mkuu wa Mkoa Mhandisi Ndikilo alimweleza kiongozi huyo kuwa, tayari Halmashauri ya Jiji la Mwanza imetenga eneo la uwekezaji katika Kata ya Buhongwa na eneo la Luchelele ambalo linasubilia wananchi kulipwa fidia ili kupisha utekelezaji wa Mji mpya wa kisasa utakaokuwa na huduma zote na kuwa limekuwa likiboresha maeneo ya Makazi na kuyauza ka Taasisi, Mashirika, Mifuko ya Hifadhi za Jamii na wananchi.

Aidha Katibu Mkuu aliyeambatana na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Jumanne Sagini na ujumbe wake, alimweleza Mhandisi Ndikilo kuwa tayari baadhi ya Wawekezaji wakubwa wameanza kuvutiwa kuja kuwekeza Jiji la Mwanza kutoka mataifa ya China na mataifa ya Bara la Ulaya kwa kuanza kuwasilisha maombi yao serikalini kupitia Balozi zao na wengine kumueleza Rais Dkt. Jakaya Kikwete .

“Lakini nikupongezeni viongozi wote kwa kushirikiana vyama na jamii na hasa mlivyoamua kutekeleza mkakati wenu wa kuwapanga katika utaratibu, kanuni na sheria wafanyabiashara wadogo maarufu kwa “Machinga” hongereni sana muendele kushirikiana na jamii, lakini inabidi viongozi wenzenu wa Mikoa yenye Majiji na Wilaya zenye Manispaa waje kujifunza kwenu juu ya utaratibu huu,”alisisitiza.

Aliongeza kuwa kutasaidia kumaliza mifarakano na wamachinga hivyo viongozi wa Majiji ya Arusha, Tanga, Mbeya na hata Dar es salamu na Manispaa zake za Ilala, Temeke na Kinondoni waje kujifunza na kuchukua uzoefu wenu ili nawao waishirikishe jamii katika kutekeleza upangaji wa Machinga hali itakayomaliza malalamiko wakati wa kuwaondosha na kuwapanga.

Balozi Sefue alitembelea eneo la mradi wa ujenzi wa jengo la kisasa la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na kupatiwa taarifa fupi iliyosomwa kwake na Katibu Tawala wa Mkoa (RAS) Ndalo Kurwijila lililokwama kukamilika kwa muda mrefu sasa kutokana na kutekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.

Ujenzi wa jengo hilo unaofanywa na Mkandarasi Kampuni ya CEF Ltd ya jijini Mwanza tangu mwaka 2008 umeshindwa kukamilika kutokana pia na Mkandarasi kudai fedha na ucheleweshwaji wa fedha zilizosalia kiasi cha Sh. Milioni 528 za ukamilishaji wake unaotokana uwasilishwaji hafifu wa fedha kwenda Hazina ndogo.

“Usanifu wa mradi wa jengo hili ulifanywa na Wakala wa Majengo wa Tanzania (TBA) na hadi kukamilika unataraji kugharimu kiasi cha Sh. Bilioni 2,635,500, 772.00 na kazi zilizosalia ni ujenzi wa ngazi kwa matumizi ya dharula, kuweka vipoza hewa, kuweka lifti ili kuwezesha watu wenye ulemavu kufika ofisi za juu, mfumo na vifaa vya moto na kuwekwa njia na bustani eneo la chini,”aliwasilisha.

Balozi Sefue alikubaliana na taarifa hiyo na kuahidi kuleta kwa wakati fedha iliyosalia ili kukamilisha ujenzi wa jengo hilo huku pia akiwaagiza uongozi wa Mkoa kuingiza kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2015/2016 mpango wa kulikarabati jengo linalotumika sasa ambalo linaonyesha kuchaka ili nalo liweze kutumika na idara zingine zitakazosalia baada ya kuhamia jengo jipya.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.