ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, June 10, 2014

MUONEKANO WA LEO KITUO CHA MWENGE JIJINI DAR KUPISHA UPANUZI WA BARABARA.

Tofauti na awali hapa zilikuwa zikionekana sura za mabasi yaelekeayo pande mbalimbali jijini Dar yakiwa katika mistari.
Chini palikuwa na sakafu ya vitofa lakini kwa sasa vimeenjuliwa na kukusanywa kama vifusi mafungu kwa mafungu. 
Ni taabu kwa abiria walikuwa na mazoea ya kupata huduma kupitia kituo hiki ambapo kwa sasa huduma zote zimehamishiwa kituo cha Makumbusho umbali wa mita kama1,000 toka kituoni hapa.
Eneo hili mbali na kuwa kituo cha daladala pia lili sheheni mishemishe mbalimbali za biashara likiwawezesha na kuwarahisishia wajasiliamali mbalimbali mamia kwa maelfu kukutana kirahisi na wateja wao kukuza vipato vyao kwa kufanya biashara na utoaji huduma mbalimbali za tija kwa wananchi wa kawaida la kini kwa sasa kweupeeeee kutoka hapa mpaka kuleee!!
Hapa kulikuwa na huduma za vyoo na kuoga!!
Majengo yaliyo salia.
Tutegemee mabadiliko gani katika muonekano wa eneo hili?
Majibu yatapatikana hapa hapa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.