ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, April 28, 2014

BUGANDO MABINGWA WA SAFARI POOL 2014 MWANZA.

Wachezaji wa timu ya Chuo cha Bugando wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa kukabidhiwa zawadi fedha taslimu Shilingi 500,000/= mara baada ya kuibuka mabingwa katika fainali zamashindano ya Safari Higher Learning Pool Competition 2014 ngazi ya mkoa yaliyofanyika Shooters pub jijini Mwanza mwishoni mwa wiki. 
Wachezaji wa timu ya Chuo cha Bugando wakishangilia kwa kucheza mara baada ya kuibuka mabingwa katika fainali za mashindano ya Safari Higher Learning Pool Competition 2014 ngazi ya mkoa yaliyofanyika mwishoni mwa wiki. 
Bugando mabingwa Safari Pool Mwanza.
Na Mwandishi Wetu.Mwanza.
CHUO cha Udaktari cha Bugando jijini Mwanza kimefanikiwa kutwaa ubingwa wa mashindano ya mchezo wa Pool ngazi ya mkoa katika mashindano ya yaliyoyoshirikisha Vyuo vya Elimu ya juu yajulikanayo kama “Safari Pool Higher Learning Competition 2014” mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa Shooters Pub.

Bugando ilifanikiwa kupata ubingwa huo kwa kukifunga chuo cha CBE 13-10, na hivyo kuzawadiwa fedha taslimu Shilingi 500,000/= pamoja na nafasi ya kupeperusha bendera ya jiji la Mwanza katika fainali za Kitaifa zinazotarajiwa kufanyika Mai 3 na 4,2014 mkoani Kilimanjaro.

Nafasi ya pili ilichukuliwa na CBE ambao walizawadiwa fedha taslimu Shilingi 300,000/=,nafasi ya tatu ni Chuo cha St.Agustin(SAUTI) ambao walizawadiwa fedha taslimu Shilingi 200,000/= na nafasi ya nne ni Chuo cha Kodi(TIA) ambacho kilizawadiwa fedha taslimu Shilingi 100,000/=

Upande wa mchezaji mmoja mmoja Wanaume,Fredrich Mwangata kutoka Chuo cha SAUTI alitwaa ubingwa na kuzawadiwa fedha taslimu shilingi 150,000/= pamoja na tiketi ya kuwalikisha mkoa wa Mwanza na mshindi wa pili ni Said Uegen kutoka chuo cha TIA ambaye alizawadiwa fedha taslimu Shiling 100,000/=.Upande wa wakinadada, Andressa Matula kutoka Chuo cha SAUTI alifanikiwa kutwaa ubingwa na kuzawadiwa fedha taslimu shilingi 100,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha wakinadada mkoa kwenye fainali za kitaifa na nafasi ya pili ilichukuliwa na Agnes Jacob kutoka Chuo cha CBE ambaye alizawadiwa fedha taslimu Shililingi 50,000/=.

Mkoani Mbeya chuo kilichofanikiwa kutwaa ubingwa wa Mkoa ni Chuo cha Mzumbe ambacho pia kilizawadiwa fedha taslimu shilingi 500,000/= pamoja na nafasi ya kuwakilisha jiji la Mbeya katika fainali za kitaifa mkoani Kilimanjaro.Nafasi ya pili ilichukuliwa na chuo cha MUST ambacho kilizawadiwa Shilingi 300,000/=,nafasi ya tatu ilichukuliwa na chuo cha TIA ambacho kilizawadiwa Shilingi 200,000/= na nafasi ya nne ilichukuliwa na chuo cha Tumaini ambacho kilizawadiwa fedha taslimu Shilingi 100,000/=.

Upande wa mchezaji mmoja mmoja wanaume, Steven Kyasi kutoka chuo cha Mzumbe alitwaa ubingwa na kuzawadiwa fedha taslimu Shilingi 150,000/= pamoja na nafasi ya kuwakilisha Mkoa wa Mbeya upande wa wachezaji mmoja mmoja kwenye fainali za kitaifa Mkoani Kilimanjaro na upande wa wakinadada, Amina Mhina kutoka chuo cha Mzumbe pia alifanikiwa kutwaa ubingwa huo na hivyo kuzawadiwa fedha taslimu shilingi 100,000/= pamoja na kuwakilisha jiji la Mbeya upande wa mchezaji mmoja mmoja katika fainali za kitaifa May 4,2014. Mkoani Kilimanjaro.

Fainali za Kitaifa zitashilikisha mikoa nane ambayo ni Iringa, Mbeya, Morogoro, Dodoma, Mwanza, Dar es Salaam, Arusha na wenyeji wa mashindano wa mwaka huu wa 2014,Mkoa wa Kilimanjaro.


Mabingwa watetezi wa mashindano hayo ya Pool vyuo yanayodhaminiwa na TBL kupitia Bia yake ya Safari Lager ni Dar es Salaam, ambacho ni chuo cha CBE.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.