ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, February 2, 2014

PAN AFRICA ENTERPRISES LTD YAKABIDHI MAGODORO KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO DAKAWA, MORO

Mkurugenzi wa Home Shopping Centre Gharib Said Mohammed (GSM) kushoto akitembea na Mku wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meki Sadiq katika daraja lilosababisha watu wa kutoka Dar kwenda Dodoma kusimama kwa muda
Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadiq akimshukuru mmoja wa wafanyabiashara wa Mkoa wa Dar es Salaam Rumin Shar kutoka kampuni ya Pan Africa Enterprises Ltd baada ya Kampuni yao kutoa magodoro 200 aina ya Comfy kwa ajiri ya ya waathirika wa mafuriko yaliyotokea wiki iliyopita eneo la Dakawa mkoani humo na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kuwaacha mamia bila makazi
Wathilika wa mafuriko wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro akimweleza kwa kina hali ilivyokuwa baada ya kutokea kwa mafuriko Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq. Nyuma katika picha ni sem trela tano zilizokuwa zimepakia vifaa na vyakula
Kamanda wa kanda maalumu ya kipolisi ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova akisalimiana na Rumin Shar kutoka kampuni ya Pan Africa Enterprises Ltd baada ya Kampuni yao kutoa magodoro 200 aina ya Comfy kwa ajiri ya ya waathirika wa mafuriko yaliyotokea wiki iliyopita eneo la Dakawa mkoani humo na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kuwaacha mamia bila makazi
Kampuni ya Pan Africa Enterprises Ltd yakabidhi magodoro kwa waathirika wa mafuriko Dakawa, Moro
Na Mwandishi Wetu, Morogoro
Kampuni ya Pan Africa Enterprises Ltd imetoa magodoro 200 aina ya Comfy kwa ajiri ya ya waathirika wa mafuriko yaliyotokea wiki iliyopita eneo la Dakawa mkoani humo na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kuwaacha mamia bila makazi.

Akikabiddhi
Jumuiya ya Wafanyabiashara wa mkoa wa Dar es Salaam wametoa vitu vyenye thamani ya shilingi milioni 117/- katika kuwasaidia wahanga wa mafuriko katika vijiji vya Magole na Mateteni vilivyoko wilaya Kilosa, mkoa wa Morogoro.

Akizungumza wakati wa kumkabidhi Mkuu wa Moka wa Morogoro vitu mbali mbali vilivyotolewa na  wafanyabiashara wa Dar es Salaam, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick alisema kuwa wafanyabiashara wa mkoa wake wameweza kutoa vitu mbali mbali kama vile nguo kwa kina mama vikiwemo vitenge na khanga.

Vitu vingine viliyotolewa na wafanyabiashara wa Dar ni pamoja na vyakula mbali mbali kama vile sukari, mchele, maji ya kunywa, unga pamoja na vyombo vya kulia chakula.

“Hali hii ya wahanga wa mafuriko imeweza kuwagusa kwa kiasi nkikubwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Dar es Salaam ambao kwa pamoja wameweza kusaidia vitu hivi vyenye thamani ya shilingi milioni 117,” alisema

Wafanyabiashara waliosaidia vitu hivyo ni pamoja na  Basic Elements kampuni tanzu ya Simon Group waliotoa tani 15 za unga wa sembe wenye thani ya shilingi milioni 15, Home Shopping Centre waliotoa mifuko 1000 ya saluji pamoja na vifaa vya kulia chakula pamoja na Pan Africa Enterprises Ltd Group ambao wametoa magodoro 200 aina ya comfy.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Joel Bendera alishukuru msaasa huo uliotolewa na wafanyabiashara hao na kusema kwamba wataugawa kwa ufasaha ili uweze kuwasaidia wahanga wote wa mafuriko.

“Tunatarajia kuugawa msaada huu wa chakula na vifaa kwa wahanga wote ili uweze kuwasaidia kwa hali na mali, mpango tulionao ni kuwapatia chakula hata cha mwezi mzima ili waweze kufanya shughuli zao nyingine kama vile kiliomo na biashara zao” alisema.


Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa kamati ya maafa ipo mbioni kutoa ripoti nzima ya maafa hayo ili kuwezesha jamii kujua athari nzima ya mafuriko hayo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.