ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 29, 2012

SAFARI YA KUKUZA VIPAJI VYA SOKA NCHINI INAANZIA MWANZA KUELEKEA NCHINI UJERUMANI



Ni mahojiano kati yetu na mkurugenzi wa kituo cha watoto wa mitaani KULEANA cha jijini Mwanza kilichojikita katika kuelimisha watoto malezi bora na suala la ukuzaji wa vipaji mbalimbali vya michezo nchini Tanzania hususani soka. Ndani ya filamu hii ya muda wa dakika 5 Mutani anatueleza mikakati na mipango kuboresha soka la nchi sanjari na mapokeo ya soka la vijana wake wa mitaani kwenye michuano ya kombe la dunia kwa vijana wa mitaani.


Timu ya Vijana wenye umri wa miaka chini ya 20 ya Tanzania Soccer Academy (TSC) yenye maskani yake jijini Mwanza iko kambini kwa sasa ikifanya mazoezi makali kujifua kwaajili ya maandalizi yake ya mwisho kuelekea nchini Ujerumani ambako itashiriki michuano kadhaa ya soka la vijana wadogo.

Vijana wakijifua kikamilifu kwa ajili ya safari.

Road to German; Frank Sekule (kulia) anaye chezea timu ya Taifa U20 anatokea kituo hiki hivyo amekuja kujumuika na wenzie kwa safari hiyo.

The Trip to German ...Seleman na Timotheo.. vijana wadogo wa squad la TSC U20.

 Majuzi katika mechi za majaribio ikicheza soka la kuvutia timu hiyo ilikichabanga kikosi kipya cha Toto Africans mabao 3-0 dimbani CCM kirumba Mwanza. Timu hiyo rasmi itaondoka nchini mnamo july 14 mwaka huu.
Kila la kheri wana wa home kila lakheri soka la Tanzania.
By G. Sengo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.