ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, February 28, 2012

LICHA YA KUPELEKA WALINZI, MABONDIA WA JIJI LA MWANZA WAWEKA HESHIMA WAREJEA NA MEDALI

Bingwa wa majiji Afrika mashariki katika Hevy Weight Dittrain Kaimbe akiwa na medali yake ya dhahabu sanjari na kombe nafasi ya tatu iliyotwaliwa na timu ya jiji la Mwanza.
Wale mabondia waliolalamikiwa na kocha wa mkoa wa Mwanza aliyetemwa kinyamela ajulikanaye kwa jina la Mgowa Haule, wanaotajwa kutoka katika kampuni ya ulinzi ya mmoja kati ya viongozi waandamizi wa timu hiyo na kuliwakilisha jiji la Mwanza kwenye michuano ya majiji iliyofanyika jijini Nairobi nchini Kenya hatimaye wamerejea nyumbani wakiwa na medali ikiwemo moja ya dhahabu ya ubingwa uzito wa juu.
Medali ya dhahabu.
Dittram Kaimbe aliyekichapa uzito wa Hevy Weight ndiye aliyeitoa kimasomaso Tanzania kwenye michuano hiyo kwa kutwaa medali ya Dhahabu huku mabondia Alex Mjakalanga wa uzito wa light welter na Daniel Wiliam wa welter wakirudi na medali za Shaba kila mmoja naye bondia wa kike Sara Andrew akirejea na medali ya Silver.

Daniel William uzito wa Welter (69) na kombe lake sambamba na medali yake ya bronz.
Kwenye mashindano hayo ushindi wa jumla ulichukuliwa na jiji la Nairobi, nafasi ya pili jiji la Kampala ile hali nafsi ya tatu ikitwaliwa na jiji la Mwanza.

Kocha wa timu ya jiji la Mwanza Omary Akida akizungumza na vyombo vya habari.

Kutoka kushoto waliosimama ni Meja Mstaafu Changarawe, bondia Alex Nyakalungu, kocha wa timu hiyo Omary Akida na Dittraim Kaimbe waliochuchumaa ni Daniel William na Sara Andrew.
Msafara wa timu hiyo uliondoka na jumla ya watu saba wakiwemo wachezaji watano, kocha na kiongozi mmoja ukiwa na kiasi cha shilingi milioni moja laki nne na elfu themanini tofauti na bajeti ya shilingi milioni 12 iliyokuwa ikihitajika.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.