ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, January 3, 2012

MVUA NEEMA - MVUA KARAHA

Mashamba katika vijiji vingi kanda ya ziwa yamejaa maji wakulima wanasema ni neema, kwani eneo kubwa la ardhi hutumika kwa kilimo cha mpunga.

Mpunga ni moja kati ya mazao yanayohitaji maji mengi katika ukuaji.

Shamba la mpunga lililooteshwa vyema, mavuno ya mwaka huu 2012 kuna kila dalili ya kupata mchele wa kutosha.

Huku Mvua zikiendelea kunyesha katika maeneo mengi changamoto iliyo kubwa ni kwamba bado wakulima wengi wanalima kwa kusuasua kutokana na kukosa mitaji ya pembejeo, mbegu na fedha kwa ajili ya utayarishaji wa mashamba kulingana na wakati, wengi mvua hizi imekuwa kama zimewashtukiza (hawakuzitegemea).

Changamoto ni kwa miundombinu ya barabara zetu wilayani na vijijini kwani nyingi si za kiwango cha lami.

Kivuko cha Mv Sengerema kunachofanya safari zake kutoka Kigongo ferry kuelekea Busisi.

Athari za mvua na ukuta wa 'Kibandaumiza' Igoma Mwanza.

Halmashauri ya jiji la Mwanza inaendelea na harakati zake kusafisha mifereji ya kandokando ya barabara ili kujizatiti kimiundo mbinu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.