Mtangazaji wa siku nyingi nchini Tanzania na mwasisi wa Shirika la Utangazaji la Tanganyika Broardcasting Cooparation (TBC) enzi hizo na Mkurugenzi wa kwanza mzawa wa Radio Tanzania Dar es salaam (RTD) Mzee David Wakati amefariki dunia alfajiri ya wa kuamkia leo jijini Dar-es-salaam katika hospitali ya Regency iliyopo maeneo ya Upanga,imefahamika.
Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa kutoka kwa ndugu wa karibu wa Mzee Wakati, mtangazaji huyo mkongwe, amefariki kutokana na maradhi ya kiarusi ambayo amekuwa akisumbuliwa nayo tangu mwaka jana. Mungu aiweke roho ya marehemu David Wakati mahali pema peponi AMEN
Marehemu David Wakati(wa kwanza kushoto) akiwa na waandishi na wanahabari wengine Ikulu jijini Dar-es-salaam walipokwenda kumuaga Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipotangaza kustaafu mwaka 1985.
Meridianbet Yawafikia Wanawake Wajane Magomeni
-
KATIKA kuendelea kutambua umuhimu wa jamii, Meridianbet leo hii iliamua
kufunga safari na kuwatembelea wanawake wajane wanaopatikana mtaa wa
Magomeni ...
RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA
-
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe.
Mwanaidi Ali Khamis akigawa iftar kwa mmoja ya mtoto anayelelewa katka
Makao ...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.