Mtangazaji wa siku nyingi nchini Tanzania na mwasisi wa Shirika la Utangazaji la Tanganyika Broardcasting Cooparation (TBC) enzi hizo na Mkurugenzi wa kwanza mzawa wa Radio Tanzania Dar es salaam (RTD) Mzee David Wakati amefariki dunia alfajiri ya wa kuamkia leo jijini Dar-es-salaam katika hospitali ya Regency iliyopo maeneo ya Upanga,imefahamika.
Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa kutoka kwa ndugu wa karibu wa Mzee Wakati, mtangazaji huyo mkongwe, amefariki kutokana na maradhi ya kiarusi ambayo amekuwa akisumbuliwa nayo tangu mwaka jana. Mungu aiweke roho ya marehemu David Wakati mahali pema peponi AMEN
Marehemu David Wakati(wa kwanza kushoto) akiwa na waandishi na wanahabari wengine Ikulu jijini Dar-es-salaam walipokwenda kumuaga Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipotangaza kustaafu mwaka 1985.
Taharuki Hoteli ya Lark, Wafanyakazi Wafungiwa nje
-
Na Mwandishi Wetu
WAFANYAKAZI 20 wa hoteli ya Lark iliyopo ndani ya jengo la Noble Centre Dar
es Salaam, linalomolokiwa na CRJE wamezuiwa kuingia ndani ya...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.