Nimetembelea Shule ya Msingi Buhangija mkoani Shinyanga ambayo hutunza watu wenye Ulemavu mbalimbali na kwa sasa imegeuzwa pia kuwa kituo cha watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino). Hapo shuleni nimekutana na Kabula Nkalango (14) mmoja wa wahanga wa mauaji ya Albino ambaye alinusulika kuuawa na wauaji kutoweka na mkono wake.
Anaomba msaada wako kumuwezesha kupata mkono wa bandia au vifaa mbalimbali vya masomo. kama uko Tayari wasiliana nami nitakuunganisha na mkuu wa shule yake.
Nae Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Babu Sikare maarufu kwa jina la Albino Fulani ambae pia ni CEO wa Afrobino akiwa katika kituo hicho cha Malezi ya watu wenye Ulemavu wa ngozi mkoani Shinyanga ambako alitembelea na kutoa misaada ya mafuta maalum kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (Sunscreen), Kofia na Mianvuli. Aliweza kuzungumza na mwanafunzi Kabula Nkalango ambaye alinusurika kuuawa katika mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi kwa kukatwa mkono wake wa kulia na kumkabidhi msaada huo kwa niaba ya walemavu wengine.
Fredrick Katulanda Mwandishi wa habari Mwananchi Communication Mwanza.
RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA
-
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe.
Mwanaidi Ali Khamis akigawa iftar kwa mmoja ya mtoto anayelelewa katka
Makao ...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.