ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 29, 2011

BARCELONA MFALME WA SOKA ULAYA FERGIE AKIRI : YAICHAPA MANCHESTER UNITED 3-1

Kocha wa Barcelona Pape Guardiola akipepezwa angani na wachezaji wake baada ya kutawazwa kuwa wafalme wa soka Ulaya kwa kuifunga Manchester United 3-1 kwenye fainali uwanja wa Wembley nchini Uingereza.

"Nilitaraji timu yangu ingefanya vizuri lakini suala ni kwamba tulikuwa tukicheza na timu bora zaidi, kitimu wako katika kilele kizuri cha mafanikio kakika mzunguko huu.

"Katika maisha yangu ya soka hakuna aliyeweza kutuficha kiasi kile, hakika ni siku kuu kwao. "Walistahili kwasababu wanacheza jinsi inavyopaswa na wanaenjoy soka lao.

"They mesmerise you with their passing and we never really controlled Messi. When we got the lifeline of Wayne Rooney I expected us to do better in the second half but it wasn't to be. Kifupi ni kwamba hakuna aibu kupoteza mbele ya wakali wale.


Boss wa Barca Guardiola amemzungumzia 'mkorofi wa chenga' Lionel Messi kwa kusema: "Lionel ni mchezaji bora ambaye sijawahiona maishani mwangu, probably the best ever. Kwani katengeneza utofauti.

"Messi ni mtu mmoja wa kipekee, Na mara zote naweka matumaini kwake kwani ni mtu asiyekata tamaa. Inapotokea akashindwa kucheza basi jua kwamba kuna kitu hakijakaa sawa katika mazingira yake yanayomzunguka. Let's hope he can continue playing well."


Huku akitokwa machozi kipa wa Manchester United aliyepanga kustaafu soka Edwin van der Sar, amesema kuwa laiti kama siku zingerudishwa nyuma angestaafu soka kabla ya mechi hiyo.









Nae Muajentina aliyeondoka Anfield kwa utata akiulazimisha uongozi wa timu ya majogoo wa London kumwachia aondoke kwenda kukiputa Barcelona katika msimu wa usajili majira ya kiangazi, JAVIER MASCHERANO. Kwa upande wake amesema "Najua kuwa mashabiki wa Liverpool bado wanahuzuni kwa kuondoka kwangu. Lakini najua hii itakuwa ni zawadi njema kwao" Akamalizia kwa kusema "You’ll never walk ’elona"

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.