Alisema hayo wakati alipokuwa akikabidhi gari la kubebea wagonjwa aina ya Nissan Patrol lenye thamani ya shs.millioni 32 katika hafla fupi iliyofanyika katika Zahanati ya Karume, iliyopo katika kata ya Bugogwa wilayani Ilemela.
Mhe.Kiwia ametoa ahadi nyingine kuwajengea wananchi wa kata ya Bugogwa, kituo cha polisi na kumuagiza Diwani wa Kata ya Bugogwa, Swila Dede Swila ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo, kata ya Bugogwa kusimamia ujenzi wa kituo hicho ambacho kitaanza kujengwa muda wowote kuanzia sasa na ujenzi wake kukamilika ndani ya siku 90.
Mbunge wa jimbo la Mbeya mjini Joseph Mbilinyi al maarufu kwa jina la Mr. sugu alikabiliwa na wakati mgumu baada ya kulazimishwa kuimba jukwaani pasipo kupanga, hiyo ni mara baada ya kuhutubia. "Tunataka UCHANE" , "CHANA MISTARI NDIYO UKAE" sauti zilisikika! Bila hiyana akawapa mistari ya kutosha ya wimbo - Wananiita sugu! ......Akashangiliwa ile mbaya na mamia yaliyohudhuria makabidhiano hayo.
Mbali na hayo, mh. Mbunge pia ameahidi kuendeleza miradi mingine ikiwemo ukarabati wa barabara, usambazaji wa maji safi kuwa itasimamiwa kikamilifu lengo likiwa ni kuleta maendeleo kwa wananchi wa kata ya Bugogwa na jimbo la Ilemela kwa ujumla.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.