Timu ya soka ya Bongo Fleva ambayo hivi karibuni iliwaangusha wenzao wa Bongo Movie kwa kuwacharaza bakora mbili kavu Siku ya Jumamosi inategemea kushuka dimbani Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kukiputa na timu ya Watangazaji na MaDJ wa Mwanza.MENEJA UWEZESHAJI WA VSS MR.MAX (KUSHOTO) AKIMKABIDHI VIFAA MENEJA MCHEZAJI WA TIMU YA WATANGAZAJI NA MADJ MWANZA DJ ALLY COCO, PEMBENI YAKE NI KAPTENI WA TIMU HIYO PHILBERT KABAGO. Katika kujiandaa na mchezo huo Kampuni ya Ulinzi jijini Mwanza ambayo pia ni moja kati ya wadhamini wa Blogu hii VSS Security Group kwa kushirikiana na club maarufu jijini Mwanza STONE CLUB jana jioni wamemwaga Ma-Full seti ya vifaa vya michezo Jezi jozi mbili, Shin guard, Sox na Viatu kwa timu ya Watangazaji na MaDJ wa Mwanza.
ALLY COCO (SHOTO) NA KABAGO MBELE YA UZI MPYA. Kiingilio kwa mchezo huo ni shilingi 2,000/= mzunguko na 3,000/= jukwaa kuu. Burudani ya muziki wa bongo fleva kutawala jukwaani kuanzia saa 6 mchana kabla ya mchezo.
Timu ya Watangazaji na MaDJ ikijifua katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kujiandaa na mchezo baina yake na timu ya Bongo Fleva Fc Jumamosi hii.
M 2tha P ambaye ni msemaji wa Bongo Fleva FC amesema kwamba timu hiyo itakuwa jijini Mwanza kwa mechi moja na timu itaambatana na nyota wake ili kulipendezesha pambano lao. Wachezaji ambao watasafiri na timu ni pamoja na Ngwear, Ben Kinyaiya, H-Baba, Soggy Doggy, Suma G, Richie One, Insepecta Haroun na Q Jay. Wengine ni KR Mullah, Z Anto, Godi Mwokozi, Kalapina, Mansu Li na yeye mwenyewe M 2tha P.
RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA
-
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe.
Mwanaidi Ali Khamis akigawa iftar kwa mmoja ya mtoto anayelelewa katka
Makao ...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.