Pichani ni moja ya kipande cha mabomu yaliyolipuka katika kambi ya jeshi la wananchi Gongo la mboto jana usiku, taarifa zinasema kuwa vipande hivi vimezagaa katika maeneo mbalimbali baada ya milipuko ya jana iliyoleta maafa ya vifo vya idadi ya watu isiyojulikana, uharibifu wa makazi ya watu na rasilimali zao.
Misururu mikubwa ya watu imeonekana ikihama kutoka maeneo ambayo jeshi limeagiza waondoke kuepuka uwezekano wa milipuko mingine kutokea.
Nikipande cha bomu Tabata Chang'ombe.
Hali bado si shwari huko Gongo la Mboto kwani bado idadi kubwa ya watoto na wakazi wa maeneo hayo wanaendelea kupelekwa uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam. Wananchi wameombwa kushiriki kwa hali na mali kuwawezesha kwa chakula, kuwasitiri kwa nguo na kwa njia yeyote wakazi hao.
”Rasmi Soko Kuu la Manispaa ya Bukoba lavunjwa”
-
Soko Kuu la Manispaa Bukoba limevunjwa ili kupisha ujenzi wa soko jipya la
kimataifa unaotarajiwa kuanza muda wowote.
Kwa Wakati tofauti wameonekana Wafa...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.