
Katika mahojiano na televisheni ya Tunisia siku ya Ijumaa, Bw Ghannouchi pia aliahidi sheria zote zisizoambatana na demokrasia nchini humo, zitafutwa katika kipindi hiki cha mpito.


Wakati huo huo vikosi vya usalama nchini Tunisia, vimejiunga na waandamanaji, katika mji mkuu Tunis. Wamesema wao ni sehemu ya watu kama walivyo wengine, na ni waathirika wa madhila kutoka kwa utawala wa zamani wa Rais ben Ali kama walivyo Watunisia wa kawaida. Hatua hii inaonekana ni maendeleo makubwa kufuatia wiki tano za harakati zilizomng'oa Rais Zine el-Abidine Ben Ali aliyeikimbia nchi wiki moja iliyopita.
Maafisa wa polisi binafsi, wanataka serikali ya mpito ijiuzulu kwa sababu imetawaliwa na viongozi waliokuwa katika utawala uliopita.
KWA HISANI YA BBC SWAHILI.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.