ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, January 9, 2011

ROY HODSON KIBARUA CHAOTA NYASI LIVERPOOL.

Kocha wa Liverpool aliye rithi mikoba toka kwa kocha Rafael Benitez mnasmo mwezi Julai mwaka 2010, Roy Hodgson (63), ameondoka uwanja wa Anfield, baada ya kushauriana na tajiri anayemilikii klabu.KOCHA MPYA KENNY DAGLISH.
Matokeo mabaya yameifanya Liverpool kuteremka hadi nafasi ya 12 katika ligi kuu ya Premier. Mchezaji wa zamani na vile vile meneja, Kenny Dalglish, atashikilia madaraka ya meneja hadi mwisho wa msimu.

"Pande zote mbili ziliafikiana kwamba kwa kuzingatia maslahi yao, ni vyema aondoke", alielezea Mmarekani anayemiliki klabu, John W Henry, kupitia maelezo katika tovuti ya klabu.


Hodgson alikataa kujibu maswali kuhusu hatma yake katika uwanja wa Anfield, baada ya Liverpool kushindwa magoli 3-1 na Blackburn, Jumatano iliyopita.Hiyo ilikuwa ni mara ya tatu kwa Liverpool kushindwa, kati ya mechi nne za mwisho ilizocheza katika ligi kuu ya Premier, hali ambayo inaifanya kuwa salama isishuke daraja, kwa kuvuka msitari huo kwa pointi nne tu zaidi.

Wakati mkutano wa Liverpool kuzungumza na waandishi ulipofutiliwa mbali siku ya Ijumaa, kuzungumzia juu ya mechi ya Jumapili ya Kombe la FA dhidi ya Manchester United, uvumi ulizuka mara moja kwamba mkataba wa kocha huyo ambaye zamani aliiongoza Fulham, ulikuwa hatarini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.