MKUU wa mkoa wa Mwanza Abbas Kandoro ameyashukia baaadhi ya makampuni binafsi ya ulinzi mkoani Mwanza kutokana na tabia yao ya kutowasilisha michango ya waajili wao katika mifuko ya hifadhi ya jamii na kuitaka mifuko hiyo kuyachukulia hatua kali ili iwe fundisho kwao.
Kwa upande wake meneja wa PPF Kanda ya ziwa Meshack Bandawe alisema kuwa PPF imekuwa ikiendesha semina hiyo kwa waajili na wadau wake mbalimbali mara moja kila mwaka kwa lengo la kukumbushana majukumu muhimu juu ya mfuko huo.
Kuhusu PPF Mkuu huyo wa mkoa wa Mwanza almeupongeza mfuko huo kwa jinsi unavyofanya kazi zake kwa ufanisi mkubwa na kutoa changamoto kwa mfuko huo kuendelea kuwekeza miradi yenye gharama nafuu kama nyumba ambazo zilijengwa mkoani Mwanza ambazo ziliwavutia wananchi wengi na kununuliwa haraka.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.