ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, January 19, 2026

NI SENEGAL BINGWA AFCON, MOROCCO YALALA NYUMBANI 1-0

 

TIMU ya Senegal ‘Simba wa Teranga’ imefanikiwa kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Morocco usiku huu Uwanja wa Prince Moulay Abdellah Jijini Rabat.


Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, kiungo wa ulinzi wa Villarreal ya Hispania, Pape Alassane Gueye dakika ya 94 katika mchezo uliodumu kwa dakika 120.


Hilo linakuwa taji la pili la AFCON kwa Senegal baada ya awali kulibeba mwaka 2021 nchini Cameroon Waliofunga Misri kwa penalti 4-2 baada ya sare ya 0-0 Uwanja wa Olembe Yaoundé.


Nyota wa Senegal, Sadio Mane wa Senegal amechaguliwa Mchezaji Bora wa michuano hiyo (MVP), Mfungaji Bora Brahim Diaz wa Morocco mabao matano, Kipa Bora Yassine Bounou wa Morocco na Timu iliyoonyesha Mchezo wa Kiungwana, Morocco. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment