ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, September 9, 2025

MWALIMU:- "NIKIWA RAIS NITAZILINDA JAMII ZINAZOIZUNGUKA HIFADHI"

 


Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Salum Mwalimu ameahidi kuweka utaratibu maalumu utakaozinufaisha jamii zinazozunguka hifadhi za Taifa endapo atachaguliwa kuunda Serikali Oktoba 29, 2025.


Akizungumza leo Septemba 9, 2025 na wakazi wa Kijiji cha Ikoma, kilichopo mpakani mwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Mwalimu amesema Serikali yake itaondoa mifumo kandamizi inayowanyima wananchi haki ya kunufaika na rasilimali asilia walizopewa na Mwenyezi Mungu.

Mwalimu amesema moja ya mikakati yake ni kuruhusu wananchi wa maeneo hayo kupata kitoweo kama swala kwa njia halali na iliyodhibitiwa, jambo analoliona kama njia ya kupunguza ujangili unaozidi kukithiri.

“Wananchi wakitaka kupata kitoweo wanaishia kupigiwa risasi kwa neema ambayo Mwenyezi Mungu alikuwa amewaruzuku. Hivi niwaulize wale wanaoishi karibu na Ziwa Victoria wanazuiwa kwenda kuvua Sangara na Sato? Yaani wao wakavue Sangara na Sato, ninyi mpigwe risasi?" amesema Mwalimu.

Akiwa anatokea Karatu mkoani Arusha alikofanya mikutano ya kampeni za kuomba kura, Mwalimu amelalamikia mfumo wa sasa, akisema unazidisha chuki kati ya wananchi na mamlaka, badala ya kushirikisha jamii katika kulinda maliasili.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment