ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, September 7, 2025

KUNDI C KAGAME LI KIBABE SANA, NA LEO TENA MECHI ZOTE DROO

 

TIMU ya Mogadishu City FC ya Somalia leo imetoa sare ya bila mabao na Kator FC ya Sudan Kusini katika mchezo wa Kundi C Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, maarufu kama Kombe la Kagame Uwanja wa KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam.
Mechi nyingine ya Kundi C Kombe la Kagame iliyotangulia mchana hapo hapo KMC Complex timu za Sudan, Alahly Wad Madani SC na Al Hilal Omdurman SC nazo zimetoka sare ya kufungana bao 1-1.
Al Hilal Omdurman SC ndio ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Sunday Damilare, kabla ya Abdelkader Ouabdi kuisawazishia Alahly Wad Madani SC.

Kwa matokeo hayo, timu zote nne zinaendelea kufungana kwa pointi mbili kila moja baada ya kila timu kutoa sare mbili katika mechi mbili za mwanzo kuelekea mechi za mwisho Septemba 10, Al-Hilal Omdurman na Kator na Mogadishu City dhidi ya Madani, zote zitaanza muda mmoja Saa 9:00 Alasiri.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment