ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 13, 2025

MGOMBEA URAIS CUF: NIKISHINDA, KEKI YA TAIFA INAWANUFAISHA WOTE

Gombo, ambaye aliambatana na mgombea mwenza wake Husna Mohammed Abdullah, alisema chama hicho kimejipanga kutenda haki kwa Watanzania wote ili wapate stahiki zao katika sekta muhimu kama afya, elimu na maji.
Gombo, ambaye aliambatana na mgombea mwenza wake Husna Mohammed Abdullah, alisema chama hicho kimejipanga kutenda haki kwa Watanzania wote ili wapate stahiki zao katika sekta muhimu kama afya, elimu na maji.

Mgombea urais wa Chama cha Wananchi (CUF), Gombo Samandito Gombo, ameahidi kwamba endapo atachaguliwa kuwa rais, atasimamia haki na kuhakikisha rasilimali za Taifa zinawanufaisha wananchi wote bila ubaguzi.

Gombo, ambaye aliambatana na mgombea mwenza wake Husna Mohammed Abdullah, alisema chama hicho kimejipanga kutenda haki kwa Watanzania wote ili wapate stahiki zao katika sekta muhimu kama afya, elimu na maji.

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu ya kugombea, Gombo alisema kwa sasa haki imekuwa ikipotea katika huduma hizo muhimu, na kwamba atakapopewa dhamana, kipaumbele chake cha kwanza kitakuwa kuhakikisha haki inapatikana kwa kila mmoja.

“Sisi kama CUF tunataka kulinda haki ya kupata huduma zote. Keki ya Taifa lazima itanufaishe Watanzania wote ili kuondoa malalamiko ya wananchi,” alisema.

Aliongeza kuwa kwa sasa kuna baadhi ya makundi ambayo yananufaika zaidi kuliko mengine, jambo linalosababisha malalamiko miongoni mwa wananchi, na CUF inakusudia kuondoa hali hiyo pindi ikishika dola.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment