HABARI IMEANDIKWA NA VICTOR MASANGU, PWANI NA KUSOMWA NA ALBERT GSENGO
Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani imesema kwamba kwa sasa bado kuna changamoto sugu kwa baadhi ya wafanyabiashara kuamua kuvunja sheria na taratibu za nchi kutokana na kupitisha biashara zao kinyemela kwa njia za magendo kupitia maeneo ya uknda wa bahari ya hindi hali ambayo inasababisha upotevu mkubwa wa mapato kwa serikali. Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa Mamlaka ya mapato Tanzania ( TRA) Mkoa wa Pwani ,Masawa Masatu wakati wa hafla ya siku ya shukrani kwa mlipa kodi kwa mwaka 2023/2024 ambapo pia amebainisha bado kuna udang'anyifu mkubwa unaofanya kwa wafanyabiashara kutumia stempu katika bidhaa ambazo ni bandia.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.