Hatimaye washindi wa Tuzo za Trace kwa mwaka 2025, wamepatikaja na kutangazwa rasmi usiku wa Jumatano Februari 26 huko Zanzibar.
Hafla hiyo iliwaleta pamoja nyota wakubwa katika tasnia hiyo kusherehekea mafanikio ya ajabu ya wasanii, watayarishaji na wasanii wa Kiafrika.
Tukio la mwaka huu liliangazia ukuaji wa ushawishi wa bara la Afrika kimataifa, huku Afrobeats, Amapiano, na aina mbalimbali za muziki za Kiafrika zikichukua nafasi kubwa.
Wasanii wawili wakali kutoka Afrika Kusini, Titom na Yuppe wametwaa tuzo ya Wimbo Bora wa Mwaka kupitia wimbo wao mkali wa ‘Tshwala Bam’, wimbo ambao umechezwa sana na wapendao burudani kote ulimwenguni kiasi cha kufanya Mdundo wao wa nguvu kuambukiza taifa na taifa hata ikawa kama utamaduni kuucheza wimbo huo.
Nyota wa Nigeria Rema ameendelea kuliteka anga, baada ya kushinda Tuzo ya Albamu Bora ya Mwaka kwa kupitia Heis, Pia ametwaa tuzo ya Msanii Bora wa Kiume, akithibitisha tena ubabe wake katika tasnia hiyo.
Katika kipengele cha Wimbo Bora wa Ushirikiano (Best Collaboration), Raia wa Ivory Coast Tam Sir & Team Paiya wameibuka kidedea kupitia mkwaju wao ‘Coup du Marteau’, wimbo wa kusisimua uliochanganya mdundo, nishati na utayarishaji bora. Wakati huo huo, tuzo ya Video Bora ya Muziki imemwendea mwana maono, mtayarishaji Meji Alabi kwa uelekezi wake shupavu wa 'DND' ya Rema.
Nguli wa Afrika Kusini Makhadzi kwa mara nyingine tena amethibitisha uwepo wake wa kipekee katika jukwaa la washindi, kwa kushinda Mchezaji Bora wa Dansi kwa maonyesho yake ya nguvu. Katika kitengo cha DJ, DJ Moh Green kutoka Algeria alitunukiwa kama DJ Bora, na hivyo kuimarisha hadhi yake kama mmoja wa wasanii wa mchanganyiko wenye ushawishi mkubwa barani Afrika.
Mkali Diamond Platnumz ameliheshimisha taifa lake na kuipeleka Tanzania duniani. akishinda kibabe kama Msanii Bora wa Kimataifa wa Afrika, huku rapa wa Ivory Coast, Didi B, akiibuka kidedea katika kipengele cha Msanii Bora wa Hip Hop kwa mtiririko mkali na kipaji chake kisichopingika.Miongoni mwa wasanii wa kike, Tyla wa Afrika Kusini alitajwa kuwa Msanii Bora wa Kike, sifa inayostahiki kwa uhalisi wake na mtindo wa kipekee ambao umevutia wasikilizaji na wapenzi wa muziki mtamu kote ulimwenguni.
Mwimbaji wa nyimbo za Injili kutoka Nigeria Mercy Chinwo ametwaa tuzo ya Msanii Bora wa Injili, kupitia kazi zake zenye kugusa mioyo zinazo ambatana na simulizi za kuhuisha na kuinua mioyo.
Washindi wa kanda ni pamoja na mwimbaji wa Ivory Coast Josey, ambaye ametawazwa kuwa Msanii Bora Anayezungumza Kifaransa, na mwimbaji wa Nigeria Ayra Starr, ambaye anaendelea kutawala Afrika Magharibi kwa sauti yake kali na nyimbo maarufu. Kusini mwa Afrika, Tyler ICU alipata tuzo hiyo, na kuthibitisha nafasi yake kama mchezaji muhimu katika eneo la muziki la kanda.
Msanii wa Kenya Bien alitambuliwa kama Msanii Bora wa Afrika Mashariki, akiwapoteza Diamond Platnumz (Tanzania), Joshua Baraka (Uganda), Harmonize (Tanzania), Rophnan (Ethiopia), Marioo (Tanzania), Zuchu (Tanzania) na Nandy (Tanzania)
Washindi wengine ni Chelsea Dinorath ya Angola aliibuka kuwa Msanii Bora Anayezungumza Kireno kwa kipaji chake kisichoweza kupingwa.
Kwa upande wa kipengele kilichokuwa kilichokuwa kikisubiriwa kwa hamu na wengi watazamaji hususani nchi wenyeji wenyewe wa tuzo, Nandy amefanikiwa kuwagalagaza wasanii wote waliokuwa kwenye kinyang'anyiro cha Msanii Bora Tanzania akiwemo Mbosso, Diamond Platnumz, Zuchu, Marioo, Alikiba, Jux na Harmonize.
IFUATAYO NI ORODHA YA WASHINDI WA TUZO ZOTE:
Tuzo za Kimataifa
Wimbo wa Mwaka
- Titom & Yuppe – ‘Tshwala Bam’ (South Africa)
- Tyla – ‘Jump’ (South Africa)
- Tyler ICU – ‘Mnike’ (South Africa)
- Tamsir x Team Paiya – ‘Coup du Marteau’ (Ivory Coast)
- Asake & Travis Scott – ‘Active’ (Nigeria)
- Tems – ‘Love Me Jeje’ (Nigeria)
- Burna Boy – ‘Higher’ (Nigeria)
- Rema & Shallipopi – ‘Benin Boys’ (Nigeria)
- Diamond Platnumz – ‘Komasawa’ (Tanzania)
Albamu ya Mwaka
- Rema – Heis (Nigeria)
- Burna Boy – I Told Them (Nigeria)
- Asake – Lungu Boy (Nigeria)
- Josey – Vibration Universelle (Ivory Coast)
- Amaarae – Fountain Baby (Ghana)
- King Promise – True To Self (Ghana)
- Stonebwoy – 5th Dimension (Ghana)
- Toofan – Stamina (Togo)
Best Collaboration
- Tamsir & Team Paiya – ‘Coup du Marteau’ (Ivory Coast)
- Titom & Yuppe & Burna Boy – ‘Tshwala Bam’ (Remix) (South Africa/Nigeria)
- Neyna & MC Acondize – ‘Nu Ka Sta Para’ (Cape Verde)
- Kocee ft. Patoranking – ‘Credit Alert’ (Cameroon/Nigeria)
- Asake & Wizkid – ‘MMS’ (Nigeria)
- Rema & Shallipopi – ‘Benin Boys’ (Nigeria)
- Odumodublvck & Black Sherif – ‘Woto Woto Seasoning’ (Ghana)
Video Bora ya Muziki
- Meji Alabi – Rema ‘DND’ (Nigeria)
- TG Omori – Kizz Daniel & Davido ‘Twe Twe’ (Nigeria)
- Director Folex – Zuchu feat Innoss’ B ‘Nani’ (Remix) (Tanzania/DRC)
- Nabil Elderkin – Tyla ‘Jump’ (South Africa)
- Kmane – Ayra Starr ‘Commas’ (Nigeria)
- Seoute Emmanuel – Toofan ‘C Pas Normal’ (Togo)
- Ach’B – Innoss’ B ‘Sete’ (DRC)
- Edgar Esteves – Asake & Wizkid ‘MMS’ (Nigeria)
Mchezaji Bora
- Makhadzi (South Africa)
- Ikorodu Boys (Nigeria)
- Dancegod Lloyd (Ghana)
- Incredible Zigi (Ghana)
- Kamo Mphela (South Africa)
- Telminho (Angola)
- Ordinateur (Ivory Coast)
- Issac Kalonji (Democratic Republic of Congo)
DJ Bora
- DJ Moh Green – ‘Kelele’ (Algeria)
- Tyler ICU – ‘Mnike’ (South Africa)
- Uncle Waffles – ‘Wadibusa’ (South Africa)
- DJ Tunez – ‘Apala Disco Remix’ (Nigeria)
- DJ Nelasta – ‘Eros’ (Angola)
- DJ Spinall ft. Tyla & Omah Lay – ‘One Call’ (Nigeria)
- DJ Neptune ft. Qing Madi – ‘Honest’ (Nigeria)
- DJ Maphorisa – ‘Mnike’ (South Africa)
- Kabza De Small – ‘Imithandazo’ (South Africa)
Best Hip Hop Artist (sponsored by Hot 97)
- Didi B (Ivory Coast)
- Nasty C (South Africa)
- Odumodublvck (Nigeria)
- Suspect 95 (Ivory Coast)
- Sarkodie (Ghana)
- Young Lunya (Tanzania)
- Maglera Doe Boy (South Africa)
Pan-African Awards
Best Global African Artist
- Diamond Platnumz (Tanzania)
- Tyla (South Africa)
- Tyler ICU (South Africa)
- Fally Ipupa (Democratic Republic of Congo)
- Burna Boy (Nigeria)
- Asake (Nigeria/USA)
- Rema (Nigeria)
- Ayra Starr (Nigeria)
Msanii Bora wa Kiume
- Rema (Nigeria)
- Dlala Thukzin (South Africa)
- Fally Ipupa (Democratic Republic of Congo)
- Diamond Platnumz (Tanzania)
- Asake (Nigeria)
- Burna Boy (Nigeria)
- Wizkid (Nigeria)
- Stonebwoy (Ghana)
Msanii Bora wa Kike
- Tyla (South Africa)
- Makhadzi (South Africa)
- Chelsea Dinorath (Angola)
- Josey (Ivory Coast)
- Ayra Starr (Nigeria)
- Tems (Nigeria)
- Yemi Alade (Nigeria)
Mtumbuizaji Bora LIVE Jukwaani
- Fally Ipupa (DRC)
- Ayra Starr – 21: The World Tour (Nigeria)
- Burna Boy – I Told Them (Nigeria)
- Tyla (South Africa)
- Yemi Alade – African Rebel Tour (Nigeria)
- Didi B – Mojo Trone Tour (Ivory Coast)
- Diamond Platnumz – Wasafi Festival (Tanzania)
Mtayarishaji Bora
- P.Priime – ‘MMS’ (Nigeria)
- Kelvin Momo – ‘Sewe’ (South Africa)
- DJ Maphorisa – ‘Mnike’ (South Africa)
- Tam Sir – ‘Coup du Marteau’ (Ivory Coast)
- Sarz – ‘Happiness’ (Nigeria)
- Jae 5 – ‘Perfect Combi’ (Ghana)
- KDDO – ‘For Certain’ (Party Next Door) (Nigeria)
- London – ‘Ozeba’ (Nigeria)
- Kabza De Small – ‘Imithandazo’ (South Africa)
Best Gospel Artist
- Mercy Chinwo (Nigeria)
- Spirit of Praise 10 (South Africa)
- KS Bloom (Ivory Coast)
- Ada Ehi (Nigeria)
- Bella Kombo (Tanzania)
- Israël Mbonyi (Rwanda)
Regional Awards
Best Artist Eastern Africa
- Bien (Kenya)
- Diamond Platnumz (Tanzania)
- Joshua Baraka (Uganda)
- Harmonize (Tanzania)
- Rophnan (Ethiopia)
- Marioo (Tanzania)
- Zuchu (Tanzania)
- Nandy (Tanzania)
Best Artist (Western Africa Anglophone)
- Ayra Starr (Nigeria)
- Seyi Vibez (Nigeria)
- Adekunle Gold (Nigeria)
- Tems (Nigeria)
- Chike (Nigeria)
- Simi (Nigeria)
- KiDi (Ghana)
Best Artist (Southern Africa)
- Tyler ICU (South Africa)
- Titom & Yuppe (South Africa)
- De Mthuda (South Africa)
- Inkabi Zezwe (South Africa)
- Dlala Thukzin (South Africa)
- Tyla (South Africa)
- Uncle Waffles (South Africa)
Best Artist Francophone Africa
- Josey (Ivory Coast)
- Didi B (Ivory Coast)
- Tidiane Mario (Congo)
- Gaz Mawete (Democratic Republic of Congo)
- Wally B. Seck (Senegal)
- PhillBill (Cameroon)
Best Artist (Lusophone Africa)
- Chelsea Dinorath (Angola)
- Calema (São Tomé and Príncipe)
- Landrick (Angola)
- Twenty Fingers (Mozambique)
- Mr. Bow (Mozambique)
- Soraia Ramos (Cape Verde)
Best Artist (Tanzania)
- Nandy (Tanzania)
- Mbosso (Zanzibar)
- Diamond Platnumz (Tanzania)
- Zuchu (Zanzibar)
- Marioo (Tanzania)
- Alikiba (Tanzania)
- Jux (Tanzania)
- Harmonize (Tanzania)
International and Diaspora Awards
Best Artist (Europe)
- Joe Dwet File (France/Haiti)
- Central Cee (United Kingdom)
- Kalash (France/Martinique)
- Darkoo (United Kingdom)
- Jungeli (France)
- Franglish (France)
- Aya Nakamura (France/Mali)
Best Artist (Brazil)
- Duquesa (Brazil)
- Racionais MC’s (Brazil)
- MC IG (Brazil)
- Péricles (Brazil)
- Tasha & Tracie (Brazil)
- Ludmilla (Brazil)
Best Artist (Caribbean)
- Lea Churro (Reunion Island)
- Venssy (French Guiana)
- Mathieu White (Guadeloupe)
- Meryl (Martinique)
- Nesly (French Guiana)
- Shenseea (Jamaica)
- Kenny Haiti (Haiti)
Best Artist (Indian Ocean)
- Barth (Reunion)
- Goulam (Comoros)
- PLL (Reunion)
- Kalipsxau (Reunion)
- Léa Churros (Reunion)
- Jamily Jeanne (Mauritius)
Lifetime Achievement Award
- D’Banj
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.