ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, January 20, 2025

JESHI LA POLISI LAMKAMATA KIJANA ALIYESAMBAZA PICHA FEKI ZA UTUPU KWA WANAFUNZI WA BAOBAO

 MWANDISHI NA. VICTOR MASANGU/PWANI

SAUTI NA. ALBERT G.SENGO


JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani limefanya msako mkali na kufanikiwa kumkamata  mtu mmoja ambaye anadaiwa kuhusika katika kutengeneza picha  za mjongeo  za utupu zenye maudhui machafu ambayo ni kinyume kabisa na maadili na sheria za nchi na kuamua kuzisambaza katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

Akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake Kamanda wa Polisi  Mkoa wa Pwani Salim Morcase amesema kwamba mtuhimiwa huyo  baada ya kufanya uchunguzi na kwamba alitengeneza picha hizo za utupu kwa kutengengeneza na kuunganisha na baadhi ya picha za majengo ya shule ya sekondari  Baobab kwa lengo la kuaminisha umma kuwa vitendo hivyo vimefanyika shuleni hapo kitu ambacho sio cha kweli hata kidogo.
  
Kwa upande wa Mkurugenzi wa Shule ya sekondari Baobab Shani Swai amekanusha vikali na kusema kwamba  kwamba wamesikitishwa sana na kitendo cha baadhi ya watu kuamua kuwachafua taasisi yao  kwa kusamabaza picha hizo za utupu  katika mitandao ya kijamii na kusababisha kuleta hali ya sintofahamu na taharuki kubwa katika maeneo mbali mbali hasa kwa wazazi na walezi.
 
Naye Kaimu mkuu wa shule taalamu Alphonce Kamisa na  Mwenyekiti wa Bodi ya Talaamu wa shule ya hiyo wamesema kutokana na jambo hilo limeweza kuleta taharuki kubwa licha ya kwamba wanafunzi tayari wamesharipoti shule kwa ajili ya kuanza na masomo yao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.