ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 16, 2024

UGANDA YAANZA KUSAFIRISHA MAFUTA KUPITIA BANDARI YA DAR ES SALAAM


 Shirika la Mafuta la Uganda (UNOC) limetangaza kuanza kutumia Bandari ya Dar es Salaam katika kupakia bidhaa hiyo kwa ajili ya kupeleka nchini kwao.


Awali UNOC ilikuwa ikitumia bandari ya Mombasa nchini Kenya katika kuchukua bidhaa hizo huku ikisafirisha kwa kutumia Shirika la Bomba la Kenya (KPC).

“Uganda imepanga kusafirisha takriban lita milioni 36 za mafuta kila mwezi (mizigo 1,028 ya lori) kupitia bandari ya Dar es salaam, “imeeleza taarifa hiyo ya UNOC iliyosainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wake, Proscovia Nabbanja

Hata hivyo, UNOC imesema kiasi hicho kinatarajiwa kuongezeka kadri siku zinavyoenda.

“Kundi la kwanza la lita milioni 18 (malori 520 ya lori) za mafuta zilianza kupakiwa wiki hii jijini Dar es Salaam na litawasili Kampala siku zijazo,”imesema taarifa hiyo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.