ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, July 18, 2024

KONGAMANO LA KWANZA LA MAANDALIZI YA DIRA YA MAENDELEO YA MWAKA 2050 KUZINDULIWA MWANZA.

 NA ALBERT GSENGO/MWANZA

Kongamano la Kwanza la Kikanda kuhusumaandalizi ya Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Mwaka 2050 litazinduliwa 20, mwaka huu jijini Mwanza huku wananchi wakitakiwa kujitokeza kutoa maoni yao.

Akizungumza na wanahabari jijini Mwanza kuhusu Kongamano hilo Mkurugenzi wa Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Thobias Makoba, amesema KOngamano hilo ni sehemu ya kuongeza uelewa kwa umma kuhusu Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050

Naye Mwenyekiti wa Timu Kuu ya Kitaalamu ya Dira ya Taifa 2050 Dkt. Asha Rose Migiro amesema wameweka tahadhari kwa kuzingatia mabadiliko ya tabia nchi na mazingira kwamba ni masuala ambayo yapo yanayoepukika na yasiyoepukika nao wamejipanga kuhakikisha malengo yatakayowekwa yanatimia kwa asilimia kubwa bila kuathiriwa. ..

Aidha Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Thobias Makoba ameongeza kuwa Kongamano hilo litaongozwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt Dotto Biteko huku likitarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Kwa Tunza Jumamosi hii, July 20, 2024 kuanzia saa 3:00 asubuhi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.