ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 29, 2024

AJALI YAUWA MASHABIKI WAWILI WA SIMBA KAMANDA AZUNGUMZA

VICTOR MASANGU/PWANI WATU wawili wamepoteza maisha na wengine watatu kujeruhiwa vibaya baada ya gari dogo la abiria aina ya Costa kupata ajali kwa kugongana na Lori katika eneo la Vigwaza Mizani Halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Pius Lutumo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo majira ya saa 12:15 asubuhi ya leo. Kamanda Lutumo ameongeza kuwa katika ajali hiyo basi dogo lililokuwa likitokea Mkoani Mbeya kuelekea Jijini Dar es Salaam lilikuwa limebeba mashabiki wa klabu ya Simba. Aidha Kamanda Lutumo aliwataja marehemu katika ajali hiyo kuwa ni Oleison Mwakasila, anaekadiriwa kuwa na miaka 42-45, mkazi wa Kiwila mkoani Mbeya na Dereva wa gari hilo dogo aitwaye Moses Mwaisela mwenye umri wa miaka (40,). Ikumbukwe siku ya jana katika eneo la bonde la mto Ruvu Wilayani Kibaha kulitokea ajali nyingine iliyohusisha magari matatu kugongana na kupelekea vifo vya watu watatu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.