ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, July 20, 2023

UWT TAIFA WAIPONGEZA NACHINGWEA KWA KUTEKELEZA ILANI YA CCM KAMA INAVYOTAKIWA

 

Mwenyekiti wa UWT taifa Merry Chatanda katika akiongea mara baada ya kukagua mradi wa RUWASA wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi na kuridhika na mchakato wake
Viongozi mbalimbali wakiongozwa na mwenyekiti wa UWT taifa Merry Chatanda wakikagua kichomea taka katika hospitali ya wilaya ya Nachingwea
Viongozi mbalimbali wakiongozwa na mwenyekiti wa UWT taifa Merry Chatanda akipata maelezo kutoka kwa mhandisi wa RUWASA Nachingwea Sultan Ndolwa akielezea namna ambavyo serikali ya awamu ya sita ikiwa na nia ya kumtua mwanamke ndoo kichwani



Na Fredy Mgunda,Nachingwea


UMOJA wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) wameupongeza uongozi wa wilaya ya Nachingwea Kwa kutekeleza miradi vizuri kama ambavyo ilani ya CCM inavyotaka.

Akizungumza wakati akikagua miradi ya maendeleo mwenyekiti wa UWT taifa Merry Chatanda alisema kuwa amekagua miradi ya maji, ujenzi wa magengo mapya katika hospital ya Nachingwea pamoja,ujenzi wa ofisi ya CCM wilaya Nachingwea na mradi wa kimaendeleo wa UWT Nachingwea wameiona inaendana na thamani ya fedha iliyotumika.

Chatanda alisema kuwa serikali ya wilaya ya Nachingwea inayoongozwa na Mkuu wa wilaya hiyo Mohamed Hassan Moyo imekuwa makini kwa kufanya kazi Kwa umakini mkubwa.

Alisema kuwa chama cha mapinduzi wilaya ya Nachingwea inafanya kazi vizuri na kwa ushirikiano mkubwa na serikali ya wilaya hiyo na kuleta maendeleo ya wananchi kama ambavyo ilivyojionea.

Mwenyekiti wa UWT taifa Merry Chatanda alisema kuwa RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Samia suluhu Hassan anafanya kazi kubwa hivyo wananchi na Wanachama wa CCM wanatakiwa kumsemea mema anayoyafanya Kwa watu ambao wanambeza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.