ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, June 12, 2023

"TANZANIA NI MOJA HAIUZIKI WALA HAIGAWANYIKI MIMI NI MTANZANIA" KAULI YA KWANZA YA RAIS SAMIA AKITUA JIJINI MWANZA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewasili mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi ya siku nne huku akisisitiza umoja katika ujenzi wa Taifa. Akisalimia na umati wa wakazi wa jiji la Mwanza waliojitokeza kumpokea eneo la uwanja wa Ndege (Air Port Mwanza) katika siku ya kwanza ya ziara hiyo, Mkuu huyo wa nchi amesema Tanzania ni nchi moja isiyogawanyika na kuwataka Watanzania kila mmoja kwa eneo lake kutimiza wajibu wa kujenga uchumi wa nchi, kisha akatia msisitizo kwa kusema "TANZANIA NI MOJA HAIUZIKI WALA HAIGAWANYIKI MIMI NI MTANZANIA"

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.