ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 17, 2023

YANGA WALEEE FAINALI SHIRIKISHO AFRIKA YAIFUMUA MARUMO NYUMBANI KWAO 1-2

 NA ALBERT G.SENGO/SPORTS RIPOTI

NGOMA imesoma Gallants Marumo 1-2 Yanga ukiwa ni mchezo wa hatua ya nusu fainali ya pili Kombe la Shirikisho Afrika. Kazi kubwa imefanywa na wachezaji wote wa Yanga wakiongozwa na Nasreddine Nabi ambaye ni Kocha Mkuu. Ni Fiston Mayele alianza kupachika bao la kuongoza kwa Yanga dakika ya 44 kisha ngoma ikapachikwa na Kenned Musonda dakika ya 67. Musonda alimalizia kazi ya Mayele na kufanya Yanga kuwa mbele kwa jumla ya mabao 4-1 kwa kuwa mchezo wa kwanza Uwanja wa Mkapa Yanga ilishinda mabao 2-1. Bao pekee la Marumo iliyokuwa nyumbani limefungwa na Chivaviro dakika ya 90 lakini ni la kufutia machozi tu. Yanga wanatinga hatua ya fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika ikiwa ni kazi kubwa kwa wachezaji na benchi la ufundi. Historia imeandikwa, hongereni Yanga, HONGERA TANZANIA

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.