ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 3, 2023

POLISI WEZI WATEKETEZWA NA WANANCHI.


Katika tukio tofauti, maafisa wawili wa polisi wameuawa na umati wenye hasira katika soko la Kanthanje, Chuka kwa wizi.

 Akithibitisha kisa hicho, kamanda wa polisi wa Kaunti ya Tharaka Nithi Zacheus Ng’eno, alisema kuwa wawili hao walipigwa hadi kufa na umati wa watu baada ya mayowe ya mmiliki wa duka la M-Pesa kuvutia watu.

Mfanyabiashara huyo alipiga nduru akidai kuvamiwa na watu wanaoshukiwa kuwa majambazi kutoka ndani ya duka lake mwendo wa saa nane usiku wa kuamkia Jumamosi, Aprili 29.

 Umati ulijibu kwa haraka kamsa hizo na kuchukua hatua ambayo ilisababisha vifo vya maafisa hao wawili wa polisi ambao wanasemekana walikuwa wamevalia nguo za raia wakati wa tukio hilo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.