ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 18, 2023

MWANAMUME MMOJA WA CHINA AMEFARIKI BAADA YA KUPIGWA RISASI NA MWINDAJI AMBAYE ALIDHANI KUWA NI SUNGURA POLISI WASEMA.


Wanaume wanne wamekamatwa kwa kifo cha Wang Moujin, ambaye alianguka kwenye shimo baada ya kupigwa risasi kichwani na bunduki ya anga.

Tukio hilo lilitokea Ijumaa iliyopita jioni wakati wanne hao walipoenda kuwinda katika Mji wa Shaxi, mkoa wa Jiangxi.

Matukio yanayohusisha bunduki ni nadra nchini Uchina.

Polisi kutoka wilaya ya Xinzhou walisema mmoja wa watu hao alifyatua risasi baada ya kuona msogeo kwenye nyasi kando ya mtaro, ambapo Bw Wang aliripotiwa kuwa akivua samaki.

Polisi waliitwa kwenye eneo la tukio na kuwakamata wanaume hao wanne, ambao baadhi yao wanafikiriwa kuwa na umri wa miaka 30.Uchunguzi unaendelea.

Uchunguzi wa maiti ulibaini kuwa Bw Wang alikufa kwa kuzama.

Uchina ina baadhi ya sheria kali zaidi za bunduki duniani, ambazo zinaweza kutumika hata kwa bunduki za kuiga au za kuchezea.

Tukio hilo limejadiliwa sana kwenye mitandao ya kijamii ya China."Inawezekanaje kwamba watu katika nchi hii wana bunduki?"Alisema mtoa maoni mmoja kwenye Weibo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.