ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 5, 2023

MWANAFUNZI AUAWA AKIENDA KWENYE MIHADI YA MPENZIWE.

 


June Jerop, mwanafunzi wa chuo kikuu cha Kenyatta aliyekuwa akisomea shahada ya uzamili katika Utawala wa Biashara alipatikana akiwa amefariki saa chache baada ya kwenda kuchumbiana na jamaa anayeshukiwa kuwa mpenzi wake.

 

June Jerop, 36 alikaa siku nzima na marafiki zake mnamo Machi 18 kabla ya kujiondoa kwenda kwenye mtoko huo. Aliwaambia rafikize kuwa atakutana na rafiki wa kiume kwenye mgahawa mahali flani lakini hakufichua mengi kuhusu hilo.

Baada ya mtoko huo simu yake ilizima na familia yake na marafiki walijaribu kuwasiliana naye bila mafanikio.

 

Mwili wake uliripotiwa kutupwa karibu na Shule ya Msingi ya Jamhuri jijini Nairobi kabla ya polisi kuhamishia mwili wake katika chumba cha kuhifadhi maiti cha City. Kulingana na polisi, mwili wake ulipatikana ukiwa umevimba na ukiwa na damu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.