ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 26, 2023

LITA BILIONI 6 ZA MAJI TAYARI ZIMEINGIZWA BWAWA LA MWALIMU NYERERE

 NA ALBERT G.SENGO/PWANI

KASI ya ujazaji maji bwawa la Mwalimu Nyerere imefikia ujazo wa lita za maji bilioni sita huku ikibaki mita kumi na tatu tu kufikia kiwango cha maji yatakayoweza kuzungusha mitambo ya kufua umeme ambapo hatua hiyo imetajwa kuwa ni kiwango kizuri kutokana na kuzidi matarajio yaliyopo katika ujazaji wa bwawa hilo. Waziri wa Nishati, January Makamba amefika kwenye mradi wa bwawa kuzalisha umeme la Mwalimu Nyerere Hydro Power Project iliopo Rufiji Mkoa wa #Pwani kukagua hatua na maendeleo mbalimbali yanayoendelea kufanyika kwenye mradi huo. Waziri Makamba amesema Maendeleo ya mradi ni mazuri kwa sasa, Na kwa mujibu wa takwimu za kiwango cha uingiaji wa maji ni kikubwa kuliko kiwango cha Maji cha mwaka 2019/2020 kilicholeta mafuriko kwa mikoa ya Pwani na Morogoro. Kasi ya ujazaji maji katika bwawa hilo inaenda sambamba na kasi usukaji na usimikaji wa mitambo ya kufua umeme pamoja na kituo cha kupokea na kusafirisha umeme. #samiasuluhuhassan #ikulumawasiliano #makamba

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.