ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 25, 2023

DARAJA LAFUNGWA BAADA YA ATHARI ZA MVUA.


Kamati ya Ulinzi Wilayani Malinyi limefunga kwa muda matumizi ya daraja la BUTU linalounganisha Tarafa za Ngoheranga na Malinyi kutokana na athari za mvua zinazoendelea kunyesha.


Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Sebastian Waryuba na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na usalama wametembelea maeneo ambayo yanatajwa kuathiriwa na mvua za masika zinazoendelea kunyesha Wilayani humo


Kulingana na kufungwa kwa daraja hilo Mawasiliano kati ya Tarafa za Ngoheranga,Malinyi na Mtimbira yamekatika.


Mkuu wa Wilaya amewashauri wananchi kipindi hiki Cha mvua wasifanye safari ambazo sio za lazima wakati serikali inaendelea kutatua tatizo la daraja BUTU.


Athari hizo za madaraja na maji kujaa katika maeneo mbalimbali zinatokana na mvua za masika zinaendelea kunyesha Wilayani humo.


Tutaendelea kukujuza kwa maeneo mengine yaliyoathiriwa na mvua hizo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.