ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, March 29, 2023

TAIFA STARS YACHAPWA 1-0 NA UGANDA DAR

 WENYEJI Tanzania wamechapwa bao 1-0 na Uganda katika mchezo wa Kundi F Kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) jana Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Bao pekee la The Cranes lililoizamisha Taifa Stars jana lilifungwa na winga wa KCCA ya nyumbani, Kampala, Rogers Mato Kassim dakika ya 90 na ushei akimalizia kazi nzuri ya Farouk Miya wa Rizespor ya Uturuki.

Matokeo hayo yanazidi kuliweka pagumu Kundi F kuelekea mechi mbili za mwisho, kwani sasa ukiondoa Algeria ambayo imekwishafuzu kwa pointi zake 12, Tanzania na Uganda zenye pointi nne kila na Niger yenye pointi mbili moja wapo unaweza kufuzu pia.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.