Mwanamume mmoja mwenye umri wa miaka 28 amekiri kuwaua wanawe wawili baada ya mke wake kuondoka nyumbani kufuatia mgomvi mkali wa kinyumbani katika kaunti ya Bomet.
Hillary
Kibet Rono anaripotiwa kuwaua watoto wake wavulana wenye umri wa miaka miwili
na mitatu kutumia upanga kabla ya kujaribu kujiua kwa kunywa sumu.
Kamanda wa
polisi wa kaunti ndogo ya Bomet ya Kati Musa Omar anasema mshukiwa anakisiwa
kulewa kulipiza kisasi baada ya mke wake kuondoka nyumbani Jumapili
Babake aliwaambia
majirani ambao walikimbia na kumkamata mshukiwa kabla ya polisi kufika.
Polisi
waliondoa miili ya watoto hao na kupata kichupa kilichokuwa na sumu
inayoaminika kunywewa na mshukiwa.
Alipewa
matibabu ya dharura katika kituo cha afya cha karibu kabla ya kupelekwa katika
Hospitali ya Rufaa ya Longisa ambako anaendelea kupata matibabu.
Polisi wamesema
kuwa mke wa mshukiwa aliondoka nyumbani wiki mbili zilizopita akihofia kuuawa
na mumewe kutokana na mizozo ya nyumbani ambayo haikuwa ikiisha.
Aliacha
wanawe wawili chini ya uangalizi wa baba yao ambaye sasa amewaangamiza.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.