ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, March 21, 2023

MWANAMKE AFARIKI DUNIA WAKATI AKISHIRIKI NGONO KICHAKANI KAUNTI YA HOMA BAY.

Mwanamme mwenye umri wa miaka 37 anakabiliwa na mashataka ya mauaji baada ya mpenzi wake aliyefahamika kama Milca na mwenye umri wa miaka 48 kufariki wakati wakifanya ngono kichakani eneo bunge la Mbita kaunti ya Homa Bay.  

Mtuhumiwa anasemekana kumrithi marehemu baada ya kifo cha mume wake kama ilivyo tamadumi ambapo mwanamke anaruhusiwa kurithiwa baada ya kifo cha mume wake

.Wawili hawa wanasemekana kuwa walionekana wakibugia pombe katika kilabu kimoja eneo hilo jioni ya kabla ya kuondoka kuelekea nyumbani.

Wakiwa njiani hapo ndipo wasia wa kuyatia mahanjam katika mapenzi yao iliwajia na kisha wakaamua kuingia kichakani eneo la Got Rateng na kushiriki tendo la ndoa wasijuwe lilokuwa linawasubiri.

Mtuhumiwa huyo aliyekutwa na kisa hicho amesemekana kuwa alijaribu kuuzika mwili wa Milca.

Kulingana na chifu wa Lambwe Mashariki Bernard Ouma wawili hawa walikuwa wameonywa dhidi ya kubugia pombe na kuwa mshukiwa hakutarajia kuwa mpenzi wake angefariki wakati wa ngono.

Amatuhumiwa huyo alikamatwa baada ya kukiri kuwa marehemu alifariki wakati walipokuwa wanashiriki ngono

Chifu wa eneo hilo amesema kuwa alikuwa amefanya kikao na wawili hao awali na kuwaonya dhidi ya hulka yao ya kufanya mapenzi kiholela  baada ya kubugia vileo.

Mwili wa mwendazake umepelekwa katika hospitali ya rufaa ya Homa Bay uchunguzi zaidi ukitarajiwa kufanywa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.