ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, March 7, 2023

MTOTO ALIYEKUWA AKIUGUA MALARIA AFARIKI DUNIA AKIOMBEWA NA PASTA ILI APONE.


Hali ya huzuni ilighubika kijiji cha Magamba Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi, Tanzania kufuatia kifo cha mtoto mwenye umri wa miaka 16.

 Consolata Charles amefariki dunia wakati alipokuwa akipokea huduma ya maombi nyumbani kwa mchungaji. 

Inaripotiwa kwamba kuwa vipimo vya awali vya hospitali vilionesha kuwa mtoto huyo alikuwa akiugua Malaria pamoja na UTI. 

Alipewa rufaa ya kwenda hospitali kubwa lakini aliruhusiwa kurejea nyumbani ambapo mlezi wake alipoamua kumpeleka kwa mchungaji kuombewa.

Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari nchini humo, wazazi wa mtoto huyo pamoja na ndugu na majirani walisema marehemu alilazwa hospitalini mara kadhaa na baadaye kuruhusiwa kurudi nyumbani. 

Lakini baada ya muda alianza kuugua tena na hali yake kudhoofika hivyo kuwalazimu wazazi wakewake kumpeleka kwa mchungaji kuombewa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.