ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 27, 2023

MAMIA YA WATU WASIOJULIKANA WAVAMIA SHAMBA LA KENYATTA


Mamia ya watu wasiojulikana wamevamia shamba la familia ya rais wa zamani wa Kenya Uhuru Kenyatta huku maandamano yakizuka nchini humo kuhusu gharama ya juu ya maisha.

Wavamizi hao walikata miti Kwa kutumia misumeno ya umeme na kuiba mamia ya mifugo kutoka kwa shamba kubwa lililo nje kidogo ya jiji kuu la Nairobi.

Sehemu kubwa ya ardhi imetengwa kwa ajili ya mradi wa makazi ya hali ya juu. Hakukuwa na polisi au vikosi vya usalama kwenye eneo hilo . Waandishi wa habari wa eneo hilo wanaoripoti uvamizi huo pia walishambuliwa na umati huo.

Biashara karibu na shamba lote zimefungwa. Kiwanda cha gesi kinachomilikiwa na familia ya kiongozi wa upinzani Raila Odinga pia kimeharibiwa katika eneo la viwanda la Nairobi.

Maandamano pia yamefanyika katika miji na majiji kote Magharibi mwa Kenya, ngome ya Bw Odinga. Waandamanaji walichoma matairi na kuziba barabara kuu katika jiji la Kisumu.

Takriban muandamanaji mmoja ameuawa katika ghasia hizo.

Bw Odinga, aliitisha maandamano nchi nzima kuhusu madai kuwa uchaguzi wa mwaka jana uliibiwa.

Pia anasema rais William Ruto ameshindwa kushughulikia gharama ya juu ya maisha nchini.

Raila, aliyekuwa Waziri Mkuu alishindwa na Bw Ruto katika uchaguzi wa Agosti mwaka jana. Aliungwa mkono na aliyekuwa rais Uhuru Kenyata

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.