ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 9, 2023

"KAZI YA POLISI SIKU YA MAANDAMANO NI KUCHUNGA RAIA" ASEMA RAILA

 

Raila Odinga amesema kazi ya polisi siku ya maandamano ni kulinda raia. Amesema hayo baada ya kuitisha maandamano kote nchini ya kushinikiza serikali ya Rais Rais William Ruto kuondoka mamlakani. 

Raila alisema siku hiyo polisi wanafaa kuhakikisha kuwa kila mwandamanaji ana usalama wa kutosha. 

 Kiongozi wa Azimio la Umoja Raila Odinga ameitisha maandamano ya umma kote nchini katika kile amesema ni mkondo wa kuiondoa mamlakani Kiongozi huyo amewataka wafuasi wake kujiandaa kwa makabiliano na serikali ya Ruto kwenye maandamano Ametaja kupanda kwa gharama ya maisha, kuteuliwa kwa jopo la kuwatafuta makamishna wa IEBC na kutofunguliwa kwa server za IEBC kama sababu ya kuanza makabiliano na Ruto.

Kiongozi wa Azimio la Umoja Raila Odinga sasa ameitisha maandamano kote nchini kushinikiza serikali ya Rias William Ruto kuondoka mamlakani.

 Kwenye kikao na wanahabari, Raila alisema sasa wafuasi wa Azimio wako huru kuandamana wakilia kuhusu machungu ya serikali ya Ruto. 

"Kuanzia leo Wakenya wanaweza kugoma, au kuandamana na kuenda katika nyumba yoyote ya serikali kupelekea malalamishi yao," alisema Raila. Raila amewataka wafuasi wake kuanza kazi rasmi leo ili kufanikisha ajenda yao. 

"Movement for Democratic Defence inaanza kufanya kazi leo," alisema kiongozi huyo wa Azimio la Umoja. Ametaja kupanda kwa gharama ya maisha, kuteuliwa kwa jopo la kuwatafuta makamishna wa IEBC na kutofunguliwa kwa server za IEBC kama sababu ya kuanza makabiliano na Rais Ruto. 

Azimio wametangaza kwamba kutakuwa na maandamano makubwa jijini Nairobi Machi 20. "Wafuasi wote wa Azimio Kenya yote watakutana jijini Nairobi Machi 20 kwa maandamano ya kukataa Ruto," alisema Raila. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.