ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 10, 2023

TAASISI YA HABARI MTANDAONI YAZINDULIWA WAANDISHI WAASWA KUACHA KUTUMIKA VIBAYA

 NA ALBERT G. SENGO/DODOMA

Hii leo Msemaji wa Serikali ya Tanzania Geryson Msigwa amemwakilisha Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye kuzindua Taasisi ya Waandishi wa Habari Mtandaoni (TOMA) . Katika uzinduzi huo uliofana ukifanyika jijini Dodoma na kuratibiwa na Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Arusha (APC) na kuhudhuriwa na wanahabari toka maeneo mbalimbali nchini, mmoja kati ya masuala yaliyochomoza kwenye hotuba na nasaha za mgeni rasmi ni pamoja na:- "Tasnia ya habari iko mikononi mwa vyombo vya habari mtandaoni, twendeni tukaoneshe weredi wa hali ya juu. Hicho ndicho kitakachotufanya tuaminike na jamii" "Ni lazima tuangalie maadili ya uandishi wa habari yanasema nini, ni lazima tuangalie sheria za nchi yetu zinasema nini, hatuwezi kuwa waandishi wa habari za mtandaoni kwa kujikita tu kwenye kuzua taharuki, kuvunja sheria aun kuchonganisha jamii na jamii au jamii na serikali" Tumetoka tulipotoka vyombo vya habari vikimilikiwa na wanasiasa na wafanyabiashara, akija mmiliki anasema weka hiki usiweke hiki. Tuacheni kutumika, hapo ndipo heshima yetu itakuwepo, fanya kazi yako kwa weredi" . . . #ikulumawasiliano #samiasuluhuhassan #dodoma #TOMA @ikulu_mawasiliano @samia_suluhu_hassan @napennauye @jembenijembe @kikotifredy @jembefmtz ZAIDI SUBSCRIBE #YouTube CHANEL YETU ILI UWE WA KWANZA KUPATA TAARIFA MBALIMBALI #Jembefmtz

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.