ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, January 10, 2023

WANAKIJIJI WAUWA FISI NANE WALIOUWA MTOTO.

 

NA ALBERT G. SENGO

Siku chache baada ya @jembefmTz kuripoti Habari ya mtoto Emmanuel Nyangela kufariki dunia baada ya kuliwa na fisi, wakazi wa kijiji cha Mwangika kata ya Mwabomba wilayani Kwimba mkoani Mwanza kwa kushirikiana na kundi maalum la kuuwa fisi wamefanikiwa kuwauwa fisi nane. Mtendaji wa Kijiji cha Mwangika, George Ernest amesema baada ya tukio hilo kutokea tarehe 27 mwezi wa 12 mwaka jana askari wa wanyapori walifika katika Kijiji hicho na kusaka fisi hao bila mafanikio hadi lilipofika kundi maalum la kuuwa fisi wakiwa wameambata na mbwa zaidi ya themanini ndipo wakafanikiwa kuwauwa fisi hao nane. "Na baada ya wao kushindwa kuuwa fisi sisi kama viongozi wa Kijiji tulikaa tukaweza kuwatafuta wawindaji wa kienyeji kutoka wilaya ya Misungwi wakaja watu kama 76 pamoja na mbwa wao wawindaji wa kienyeji ni watu ambao wanawinda kwa njia za asili kwa kutumia dawa za kienyeji na walitumia siku nne na wakauwa fisi wanane" amesema Mtendaji huyo wa kijiji cha Mwangika, George Ernest.
#DriveMix . . . . #2023Kimewaka

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.